Posts

Showing posts from May, 2025

DIWANI MWASHITETE AYATAJA MABILIONI YA RAIS DKT,SAMIA YALIVYOING’ARISHA KATA YAKE

Image
MAKALA ‘’Wanaomsema vibaya Rais Dkt,Samia wakapimwe akili,amegusa kila sekta kujenga miradi,imeturahisishia kupunguza hoja kwa wananchi wakati wa kuomba kura’’. Na Ibrahim Yassin,Songwe DIWANI wa kata ya Harungu wilayani Mbozi mkoani Songwe Maarifa Mwashitete,amemsifu Rais Dkt,Samia Suluhu kwa kujenga miradi iliyogusa jamii katika idara zote huku akiwaponda wanaomsema vibaya Rais akidai kuwa wakapimwe akili. Mwashitete aliyedumu nafasi hiyo kwa mihura miwili ambapo miaka mitano iliyopita alikuwa diwani kupitia chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) ambapo pia alikuwa mwenyekiti wa vijana mkoani humo,alipohamia CCM aliukwaa tena udiwani. Alisema kata yake ina vijiji 6,vitongoji 31 ikiwa na wakazi zaidi ya 30,000 ambao awamu zilizopita walikuwa wakikabiliwa na changamoto nyingi zilizopatiwa majibu katika awamu ya sita,kwa kujengewa miradi sekta zote. Alisema katika utawala wake wa miaka mitano chini ya Rais Samia kata yake imenufaika zaidi kwa kuletewa mabilioni ya fedha kujenga mir...

WANAFUNZI WACHEKELEA DARASA LA MAABARA KUSHEHENI VIFAA,WAMTAJA RAIS DKT,SAMIA.

Image
Na Ibrahim Yassin,Mbozi ‘’Ilikuwa ngumu wanafunzi kupenda masomo ya Sayansi kutokana na kutokuwepo kwa vifaa,baada ya Rais Samia kutupa vifaa wanafunzi wanayapenda masomo,ufauru umeongezeka,diwani Mwashitete akiwezesha vyakula’’ UKOSEFU wa Darasa la maabara na vitendea kazi vya kujifunzia kwa vitendo masomo ya Sayansi chanzo wanafunzi nchini kutoyapenda masomo ya Sayansi,imeelezwa. Masomo ya Sayansi yanaumuhimu mkubwa kwa wanafunzi ambapo baadhi ya wanafunzi wanagoma kuyasoma masomo hayo wakidai ni magumu na kupelekea kuchagua masomo mengine. Kutokana na hali hiyo,Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt,Samia Suluhu imeweka utaratibu mzuri wa kujenga madarasa mapya yakiwemo ya Maabala na vifaa vyake hali iliyorudisha hali kwa wanafunzi kuanza kuyapenda masomo hayo. Mwandishi wa kituo hiki jana alifika katika wilaya ya Mbozi mkoani Songwe na kutembelea shule zilizopo kata ya Harungu na kujionea darasa la maabara likisheheni vifaa muhimu vya kujifunzi kwa matendo wanafunzi. Jeremiah ...

KASI YA KATAZO LA UHARIBIFU WA MAZINGIRA KWENYE VYANZO VYA MAJI UONGEZEKE.

Image
MAKALA ---TUTUNZE MAZINGIRA NA KUACHA KUKATA MITI YA ASILI KWENYE VYANZO VYA MAJI KULINDA UOTO WA ASILI NA KUSABABISHA UKAME--- Na Ibrahim Yassin,Songwe ‘’Lengo ni kufikia asilimia 90 kutoka 83 iliyopo,kuna mradi wa Bilioni 119 uliosainiwa na Waziri wa fedha na waziri wa maji chanzi ni mto Momba,wakazi wa majimbo ya Tunduma,Momba,Mbozi na Mlowo watanufaika’’  UKAME na uhaba wa mazi unatokana na uwepo wa uharibifu wa mazingira kwenye vyanzo vya maji vinavyofanywa na baadhi ya watu kufanya shughuri za kibinadamu kwenye vyanzo hivyo kwa kulima,kukata miti ama kuingiza mifugo. Maji ni muhimu kwa viumbe vyote duniani, bila maji hakuna uhai,aidha maji ni muhimu kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii, Kiwango cha maendeleo ya jamii yoyote kinategemea kuwepo kwa maji ya kutosha na yenye ubora unaotakiwa.  Katika hali yake ya asili, maji ni sehemu ya mazingira ambapo wingi na ubora wake ndio unaosaidia katika kuamua jinsi maji yatakavyotumika. Upatikanaji wa maji safi na salama kwa ajili ya matum...

WANANCHI WAIPA 5 SERIKALI YA AWAMU YA 6 KUFANIKISHA KUSAMBAZA UMEME VIJIJI VYOTE.

Image
Na Ibrahim Yassin,Songwe MPANGO wa serikali kuhakikisha vijiji vyote vinapatiwa umeme umetimizwa baada ya wananchi kumueleza katibu tawala mkoani Songwe alipokuwa wilayani Songwe. Awamu za nyumba hali ya upatikanaji wa umeme ulikuwa ni ndoto lakini mkakati ulianzia awamu ya 5 chini ya Hayati John Magufuli na ilipofika awamu 6 chini ya Rais Samia Suluhu tayari vijiji vyote vimepatiwa umeme. Wananchi hao walimueleza Katibu tawala alipotembelea miradi wilayani Songwe kuwa awapelekee salam kwa Rais Samia kutatua kero ya umeme wakisema watamlipa kura za ndiyo katika uchaguzi mkuu ujao. Mariet Mwashilindi mkazi wa Songwe alisema ana kila sababu kuipongeza serikali kwa kutimiza ahadi yake ya kila kijiji kuwa na umeme hivyo aliomba ahadi hiyo itimizwe ngazi ya vitongoji ili wananchi wajiinue kiuchumi. Sharif Mtambo mkazi wa kata ya magamba,alisema alisema kuna vitongoji kadhaa havina umeme aliomba watimiziwe ili waanze kufunga mashine za kusaga nafaka na salooni ili waingize kipato na kuubores...

SERIKALI YATENGA BILL, 6 KUJENGA DARAJA LA MSANGANO MTO NKANA KUKUZA RURSA ZA KIUCHUMI.

Image
Na Ibrahim Yassin,Momba WANANCHI wa vijiji vilivyopo katika bonde la Msangano wilayani Momba mkoani Songwe,wameanza kupata manufaa ya kukuza uchumi wao kutokana na serikali ya Rais Dr, Samia Suluhu kujenga daraja katika mto Nkana kuunganisha wakazi wa Momba –Tunduma hadi makao makuu ya mkoa. Wananchi wa Bonde la Msangano asilimia 75 wanategemea kilimo,ufuga ji na uvuvi kuendesha maisha yao ya kila siku ambapo kwa miaka mingi walikumbwa na kadhia ya kusafirisha bidhaa zao kupitia njia ya Sumbaw anga mkoani Rukwa hadi kufika Tunduma –Mbozi na mkoawa Mbeya k utokana na ukosefu wa daraja. Baada ya kero hiyo ya Muda mrefu,serikali ya Rais Dr,Samia ilisikia kilio cha wananchi na kutoa kiasi hicho cha fedha kujenga daraja hili kuwaon dolea wananchi kero iliyodumu zaidi ya miaka 20. Wakizungumza jana wakati wa ziara ya katibu tawala wa mkoa wa Songwe,wakazi hao walisema Rais Dr,Samia ameingia katika kitabu cha kumbukumbu kwa kuwezesha ujenzi huo ambapo wakati wakandarasi wanaanza walidhani ni ...

Uwazi wa mapato na matumizi ya kijiji chawa kichocheo kwa Wananchi kushiriki shughuli za maendeleo

Image
Mwenyekiti wa kijiji cha Swahila Legius Choma Na Israel Mwaisaka, Rukwa Wananchi wa Kijiji cha Swahila kata ya Mkwamba wilayani Nkasi wameridhishwa na uwazi unaofanya na viongozi wao wa Kijiji katika kuweka wazi mapato na matumizi kitu kinachowafanya wao kujitokeza katika shughuli mbalimbali za maendeleo ya kijiji. Wakizungumza na Majira Wananchi hao walisesema kuwa hivi sasa wanajenga shule mpya ya msingi shikizi kwa njia ya kujitolea ikiwa ni pamoja na kuongeza ukubwa wa jengo la zahanati ya kijiji hicho na kuwa tayari kutoa michango mbalimbali ya kufanikisha shughuli hizo na kuwa michango yote wanayoitoa matokeo yake wanayaona na uwazi uliopo unawafanya kuendelea kujitolea kufanya kazi za maendeleo. Sophia Kambaulaya,Edigar Minazi na Judithi Kipeta kwa niaba ya Wananchi hao wamedai kuwa katika siku za hivi karibuni wameguswa na utaratibu wa kujitolea kwenye shughuli za maendeleo kutokana na uwazi uliopo wa viongozi wao na kuwa hivi sasa uongozi wa Kijiji umekuwa ukiwasomea mapato n...

UWANKA yapata viongozi wa muda kwa kipindi cha miezi sita

Image
Na Israel Mwaisaka, Nkasi Umoja wa Watumishi Nkasi UWANKA umepata viongozi wa mpito watakaouongoza Umoja huo kwa kipindi cha miezi sita. Viongozi hao Moja ya jukumu kubwa walilonalo ni kujenga umoja huo na kuweka misingi itakayotumika ikiwa ni pamoja na kuandaa uchaguzi mkuu kwa mujibu wa katiba ya umoja huo na kupata viongozi wa kudumu. Waliochaguliwa ni Mwenyekiti Didas Saadan,Makamo mwenyekiti Beatrice Mlay,Katibu mkuu Victor Makoba na mweka hazina Abbas Kiloge. Kwa mujibu Afisa utumishi wa halmashauri ya wilaya Nkasi Rainel Mwenda kwa niaba ya mkurugenzi Mtendaji Afraha Hassan ni kuwa umoja huo dhumuni lake kubwa ni kusaidiana wakati wa shida ikiwa ni pamoja na kuleta ushirikiano na umoja mahala pa kazi. Ili mtumishi aweze kuwa mwanachama wa umoja huo atalazimika kujiunga kwa kiingilio cha Tshs,20,000 na zoezi Hilo limeanza sasa Hadi Juni 25,2025. Mwenda amedai kuwa umoja huo kama utakwenda sawa na malengo waliyoyaweka huenda wakaenda mbali Zaidi kwa kutengeneza ushirika wenye ngu...

Wananchi wafurahishwa kukamilika kwa mradi wa maji huku wakihitaji umeme kukuza uchumi

Image
‘’Baada ya mradi huu kukamilika hakuna tena shida ya maji,ila tunaomba umeme,program ya serikali ya kila kijiji kuwa na umeme sisi hatujafikiw a,tunashindwa kuwa na kasi ya kiuchumi’’ Na Ibrahim Yassin,Songwe WAKAZI wa kijiji cha Songambele kata ya Magamba wilayani Songwe mkoani hapa, wameanza kunufaika na mradi wa maji wa program ya serikali ya kujenga visima 900 nchi nzima ambao kwa kila jimbo kuchi mbiwa visima vitano na wao wakiwa ni wanufaika lakini wameomba wawekewe umeme kuongeza tija. Kijiji cha Songambele kipo mpakani na vijiji viliyopo wilaya ya Mbozi,amba cho tayari kimeondokewa na uhaba wa maji ambapo kwa sasa hitaji lao kubwa ni umeme ili waweze kujenga miradi ya kibiashara kuongeza tija za kiuchumi. Wakizungumza mwishoni mwa wiki,wakazi hao walisema awali walipata hadha kubwa ya maji na kulazimika kugombaniana na Ng’ombe maji ya kwnye madimbwi ambayo hata hivyo si safi na salama hali iliyosababisha waugue homa za matumbo. Jesto Mgaza mkazi wa kijiji cha Songambele,alisema...

Kituo cha afya Kapele chaleta furaha kwa Wananchi,Rais Dkt,Samia atajwa kwenye mafanikio hayo

Image
‘’Nilishuhudia mwaka 2018 dada yangu Aide Simkamba,akipoteza maisha akiwa njiani akikokotwa na baiskeli kwenda kujifungua kata ya Ikana kilometa 56, Rais Dkt,Samia ametufuta machozi’’ Na Ibrahim Yassin,Momba Wananchi wa vijiji vilivyopo kata ya Kapele wilayani Momba mkoani Songw e wamemtaja Rais wa Tanzania Dkt,Samia Suluhu kuwa amewafuta macho zi baada ya kuwajengea kituo cha afya kinachotajwa kuwa mkombozi kwao baada ya ndugu zao kupoteza maisha wakitembea umbali mrefu kusaka tiba. Kituo hicho cha afya kipo katika Tarafa ya Ndalambo ikiwa na vijiji 8 vyenye idadi ya watu25,442 kati ya hao wanaume ni 12,391 wanawake wakiwa 13,051 huku ikiwa na kaya 5,287. Kutokana na idadi hiyo kuwa kubwa ,wakazi hao walianzisha ujenzi wa kituo hicho baada ya kuchoshwa kutembea umbali wa kilometa zaidi ya 50 hadi kituo cha afya Ikana hali iliyosababisha wanawake kuzalia njiani na wengine kufariki. Baada ya kuanza ujenzi huo,halmashauri ya wilaya ya Momba iliomba fedha serikali kuu na mwaka 2018 walipo...

RAS -SENEDA ARIDHISHWA NA UJENZI JENGO LA UTAWALA HOSPITALI YA WILAYA YA SONGWE.

Image
Na Ibrahim Yassin,Songwe KATIBU Tawala mkoani Songwe Happines Seneda,ameridhishwa na ujenzi wa miundombinu ikiwemo jengo la utawala katika hospitali ya wilaya ya Songwe baada ya kufanya ukaguzi akiwa na wataalam kutoka mkoani. Hospitali ya wilaya ya Songwe ni miungoni mwa hospitali 67 za awali katika mpango wa maboresho ya miundombinu ya kutolea huduma za Afya nchini na utekelezaji wake ulianza Mwezi Machi 25/2019 ambapo fedha zilitolewa kwa awamu 7. Jumla ya Tsh,Bilioni 3.785 za Uviko zilitolewa na serikali kuu na zilitolewa kwa awamu 7 zikijenga majengo 17 kwa mtindo wa Force Accaunt na majengo yote muhimu yalijengwa kilichosalia ni ukamilishaji wa baadhi ya miundombinu na jengo la utawala likiwa asilimia 99. Akizungumza jana na mwandishi wa Habari hizi,Mganga mkuu wa hospitali ya wilaya hiyo.Dkt,Kalvin Mwasha alisema Pmoja na ukamilishaji wa majen go hayo,pia walipokea fedha Tsh,Milioni 400 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba kwa awamu mbili. Alisema mwaka 2024-25 hospitali ilipokea ...

BIL,7 KUJENGA DARAJA KUUNGANISHA MOMBA NA MBEYA,WAKULIMA WACHEKELEA.

Image
Na Ibrahim Yassin,Songwe WANANCHI wa vijiji vilivyopo bonde bonde la Kamsamba wilayani Momba mkoani Songwe,wameiponge za serikali kwa kusikia kilio chao kwa kuwajengea daraja kubwa linalounganisha vijiji vya bonde la Kamsa mba hadi Mlowo kuelekea Mbeya.               Bonde la Kamsamba linatumika kwa kilimo cha mazao mbalimbali ambapo wakulima watarahisishiwa kusafirisha mazao ya nafaka na samamki ambapo awali walitumia njia ya mzunguko kusafirisha bidhaa hizo kwa bei kubwa. Wakizungumza jana wakati wa ziara ya kikazi ya katibu tawala mkoani Songwe wakazi hao walisema kukamilika kwa daraja hilo kutaongeza fursa za kiuchumi na hata kuipa wilaya yao sura mpya kutokana na kutokuwa na barabara ya Lami. Isack Mkumbwa mkazi wa Kamsamba alisema walilazimika kusafirisha mazao kupitia njia ya Sumbaw anga Tunduma hadi Mbeya wakitumia fedha nyingi kutokana na ukosefu daraja katika barabara hiyo na kwamba mradi ukikamilika fursa za kiuchumi zitaongezeka. Samwel Sinkala mkazi na mkulima wa Msangano,...

Mradi wa maji Myunga kunufaisha watu 5,000 kuepuka kunywa maji yaliyochanganyikana na mizoga

Image
Meneja wa Ruwasa mkoani Songwe Charles Pambe akiwa kwenye moja ya miradi ya maji wilayani Momba,(Picha na Ibrahim Yassin Na Ibrahim Yassin,Momba ‘’Tulikunywa maji ya mto yaliyopo kilometa 3 kutoka hapa,yaliyochanganyi kana na vinyesi,mizoga kwa muda mrefu,tuliuguma homa za matumbo na kuharisha,Rais Dkt,Samia ametukomboa tutaulinda mradi huu’’ WAKAZI Zaidi ya 5,000 wa vijiji vilivyopo kata ya Kapele wilayani Momba mkoani Songwe,wamehepuka na na kadhia ya kunywa maji ya mto Momba yaliyochanganyikana na mizoga ya Wanyama baada ya serikali kujenga mradi wa maji safi na salama. Wilaya ya Momba ni moja ya wilaya iliyokuwa ikikabiriwa na uhaba mkubwa wa maji safi kwa miaka ya nyuma hali iliyowalazimu kunywa maji ya kwenye madimbwi Pamoja na mifugo,lakini ujio wa Rais Dr,Samia wamehepukana na kadhia hiyo. Consolata Sikamanga mkazi wa Kijiji cha Myunga jana alisema awali walikuwa wakitembea umbali wa kilometa 3 hadi kwenye mto Momba,maji ambayo yalichanganyikana na vinyesi,mizoga watu walifua ...

BARABARA ILIYOAHIDIWA NA HAYATI DR,MAGUFULI YAANZA KUJENGWA KUING’ARISHA WILAYA YA SONGWE.

Image
Na Ibrahim Yassin,Songwe WANANCHI wilayani Songwe mkoani hapa wameanza kutabasamu baada ya wakala wa barabara za vijijini na mijini (Tarura) wilayani humo,kuanza ujenzi wa barabara ya kiwango cha Lami yenye urefu wa kilometa 4.0 itakayoiweka katika sura nzuri mji wa Mkwajuni. Ujenzi wa barabara za Lami mkwajuni mjini ni utekelezaji wa ahadi ya aliyekuwa Rais wa awamu ya tano Hayati Dr,John Magufuli wakati wa kampeni za uchaguzi mwezi Octoba 2025 akiwa wilayani humo alitoa ahadi hiyo. Akizungumza jana wakati wa ziara ya katibu tawala mkoani humo, meneja wa wakala wa barabara mijini na vijijini (TARURA) Mhandisi Emmanuel Nkwera alisema mpaka sasa wamefanikiwa kujenga kilometa 2.87 kwa kiwango cha Lami na kuwa kukamilika kwa barabara hiyo itapelekea kuwa na barabara zenye urefu wa Kilometa 4.87. Alisema ujenzi huo wa barabara za Mkwajuni zenye kilometa 2.0.Barabara ya Pangani Mita 320,Mdula Mita 410,Moravian 1 mita 240,Moravian 11 mita 320 unatekelezwa kwa fedha za tozo ya mafuta kwenye T...

BIL,6 ZA RAIS SAMIA KUJENGA MRADI WA MAJI MOMBA WANANCHI WAPAGAWA.

Image
Na Ibrahim Yassin,Momba WANANCHI wa vijiji vitatu vilivyopo kata ya Msangano wilayani Momba mkoani Songwe,wameanza kupata matumaini ya kuondokana na kero ya maji baada ya serikali kujenga mradi mkubwa wa Msangano Naming’ongo kujengwa.     Wakazi wa maeneo hayo jana walimueleza katibu tawala wa mkoa wa Songwe,kuwa mradi huo utakapo kamilika utakuwa ni muarobaini kwao kwani wamekuwa wakitumia maji ya kwenye madimbwi kwa muda mrefu ambayo si safi na salama. Sophia Silumbwe mkazi wa Msangano,alisema tatizo la ukosefu wa maji liliwasumbua muda mrefu walilazimika kutembea kilometa 4 kusaka maji ya kwenye madimbwi,hivyo aliiomba serikali kuharakisha mradi huo ili waanze kunufaika. Julias Mtafungwa mkazi wa Naming’ongo’ alisema wametumia maji yasiyosalama kwa muda mrefu na kuugua homa za matumbo huku wakiwa na ugomvi wa kindoa baada ya wake zao kutoka usiku wa manane kusaka maji,hivyo mradi huo utakuwa ni mkombozi kwao. Akizungumza wakati wa ziara ya katibu tawala mkoani humo.Kaimu meneja wa w...