Posts

Showing posts from August, 2024

BARAZA LA KILIMO TANZANIA ACT LATOA MISAADA KWA VIJANA MKOANI RUKWA

Image
Na Baraka Lusajo,Rukwa Baraza la kilimo la Taifa Tanzania kwa kushirikiana na shirika la USAID limekabidhi msaada wa vitendekea kazi kwa vijana wilayani Kalambo mkoani Rukwa ikiwemo mtambo wa kuchakata mahindi mashambani pamoja na pikipiki moja ambavyo vitawawezesha vijana kulima na kuzalisha kwa tija. Msaada huo wenye thamani ya 4000 dollors za Kimarekani umekabidhiwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kalambo Daud Sichone kupitia hafla iliofanyika katika Ofisi za Mkurugezi Mtendaji Halmashauri ya Kalambo na kushuhudiwa na Afisa Mradi kutoka Baraza la Kilimo Tanzania Bi.Beth Musa na kumkabidhi Moses Simuyemba mkazi wa Kijiji cha Ilambila wilayani Kalambo. Mwenyekiti wa Halmashauri  Daudi Sichone amesema lengo la Serikali ni kuwawezesha vijana kiuchumi  na kusisitiza vijana kufanya kazi kwa bidhii ikiwemo kujikita kwenye shughuli za uzalishaji hasa katika Kilimo ili kuendelea kunufaika na miradi ya serikali na hatimaye kufikia malengo yao. Kaimu mkurugenzi mtendaji Halamashauri ya Kalambo...

NFRA Yawatahadharisha Vishoka ununuzi wa mahindi wao wapanga kununua tani 137,000

Image
Na Ibrahim Yassin,Songwe WAKATI wakala wa chakula nchini (NFRA) ikiendelea kununua mahindi ya wakulima mkoani Songwe madalali au vishoka wanaowadalalia wakulima wamepewa angalizo la kutombughudhi mkulima. Serikali kupitia wakala wa chakula nchini imepanga kununua tani 137. 000 za mahindi ya wakulima ambapo kilo 1 inanunuliwa kwa Tsh, 700 na hadi jana tani 28.000 zimekwisha nunuliwa. Hata hivyo katika zoezi hilo kulikuwepo na viashiria vya madalali kujipenyeza kuwalaghai wakulima lakini hilo limedhibitiwa na wakulima wanaouza mazao yao kwa amani. Akizungumza leo Agosti 29/8/2024 meneja wa kanda wa wakala wa chakula nchini Jofrey Lupenza amesema zoezi la ununuzi linaendelea vyema na wanatarajia kununua tani 137.000 za mahindi huku tani 28.000 zikiwa tayari zimenunuliwa. Alisema mahindi waliyonunua awali nchi ya Zambia wameiuzia Tani 55.000 na wanatarajia kuyabeba siku yeyote kuanzia leo na kwamba muitikio wa wakulima kuwauzia mahindi upo vizuri ukilinganisha na ilivyokuwa awali. Alionge...

Chuo cha DIT kupata kituo cha Polisi RPC aongoza kikao kuweka mikakati

Image
Na Ibrahim Yassin.Songwe Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Augustino Senga ameongoza Kikao kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi wa Kituo cha Polisi katika Chuo cha D.I.T kilichopo Kijiji na Kata ya Myunga, Wilaya ya Momba. Kikao hicho kimefanyika jana Agosti 27, 2024 katika Ofisi ya Mkuu wa Chuo Dkt.Lujaji Makamo ambapo kituo hicho cha Polisi kitajengwa katika eneo la chuo kwa ushirikiano kati ya Chuo, Wananchi wa eneo hilo pamoja na Jeshi la Polisi. Kamanda Senga amesema Lengo la kujenga kituo hicho ni kuimarisha usal ama wa mali za Chuo na Wananchi wa maeneo jirani na kuongeza hali ya usalama wa raia na mali zao. Aidha, Kamanda Senga ameongeza kuwa lengo la ujenzi huo utaanza mara baada ya taratibu za kura thimisha ardhi utakapokamilika ambao upo kwenye mchakato mzuri. Sambamba na hilo, Dkt Makamo amelishukuru Jeshi la Polisi kwa kuendelea kushirikiana na taasisi mbalimbali katika jitihada za kubaini, kuzuia na kutanzua uhalifu na wahalifu i...

M-NEC MWASELELA AINGIA KWENYE HISTORIA NZITO ATOA AJIRA KWA VIJANA.

Image
Na Ibrahim Yassin,Songwe  MJUMBE wa Halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM)  Mkoa wa Mbeya  Ndele Mwaselela (MNEC) jana ametoa ajira kwa vijana watano wa Umoja wa Vijana wa CCM wilaya ya Mbeya Mjini. Mwaselela ambaye pia ni mkurugenzi wa shule za Patrick Mission High School, Paradise Mission Pre and Primary School na Chombo cha habari kinachotambulika kwa jina la Umoja Tv. Ajira alizozitoa ni za waalimu wawili, waandishi wa habari wawili, pamoja na fundi umeme mmoja ambapo ajira za vijana hao amezitoa papo hapo alipokutana nao kwenye kikao kazi. Amesema Walimu hao wataanza kazi katika shule ya msingi ya Paradise akiwemo Mwalimu wa Lugha na Mwalimu wa Michezo pamoja na fundi wa umeme. Amesema waandishi watakaoajiriwa mmoja atafanya kazi katika Ofisi ya Umoja Tv na mwingine atafanya kazi ya Mawasiliano na mahusiano ya umma katika shughuli zake binafsi. Aidha Mwaselela mbali na kutoa ajira hizo pia amewaasa vijana kuchangamkia fursa mbalimbali zikiwemo za ajira ili wajipatie kipato n...

NANYARO AWAASA VIJANA KUTOKAA VIJIWENI KUPIGA SOGA AWATAKA WAJIUNGE KWENYE VIKUNDI VYA UZALISHAJI MALI.

Image
Na Ibrahim Yassin,Songwe  VIJANA nchini wametakiwa kutokaa vijiweni kupiga soga za umbea na badala yake wajiunge au waanzishe vikundi vya uzalishaji mali na kukop esheka vitakavyo waondoa kwenye lindi la umasikini. Kauli hiyo imetolewa leo Agosti 28/2024 na mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM mkoani Songwe Alipozungumza nao katika kata za Msangano Tindingoma na Mkulwe wilayani Momba mkoani Songwe. Alisema imekuwa ni kawaida vijana kupenda kukaa vijiweni badala ya kujiingiza kwenye utafutaji fedha kupitia kilimo,Uvuvi, Ufugaji Viwanda na biashara na kwamba uenda wanafanya hivyo kutokana na kukosa watu wa kuwashika mkono. Nanyaro ambaye pia ni mdau wa maendeleo wa nyanda za juu kusini aliwataka vijana hao kuunda vikundi na kujisajiri ili waweze kupata mikopo ya halmashauri na hata ya kwenye taasisi za kifedha na kuanzisha miradi. "Undeni vikundi mvisajili anzisheni miradi mimi kama kiongozi nitawapambania mpate mikopo na kizuri zaidi Rais Dkt Samia Suluhu amerudisha ile mikopo ya asili...

Maafisa Ugani Ileje wakabidhiwa vitendea kazi,wamshukuru Rais Samia

Image
Na Ibrahim Yassin,Songwe Maafisa Ugani katika Halmashauri  ya Wilaya ya Ileje mkoani Songwe wametoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu kwa kuwapatia vitendea kazi ikiwemo Vishikwambi, Gwanda pamoja na Pikipiki. Akizungumza leo Agosti 28/2024 wakati wa kukabidhi vifaa hivyo Mkuu wa Wilaya ya Ileje Farida Mgomi amewasihi Maafisa hao kuvitendea haki vifaa hivyo ili viweze kuleta tija na mapinduzi ya kilimo wilayani humo. Amesema pia vitasaidia kuweka msukumo mkubwa katika kuhakikisha wananchi wanazalisha mazao ya kimkakati na kibishara ikiwemo mazao ya Kakao, Pareto, Iliki pamoja na Kahawa. Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje Nuru Waziri Kindamba ametoa rai kwa Maafisa hao kuhakikisha wanasimamia na kutoa elimu ya kitaalamu hususan kwa wakulima ngazi ya vijiji katika suala zima la uzalishaji wa mazao. Kindamba amesema hali ya hewa ya Wilaya hiyo inaruhusu uzalishaji wa mazao ya aina mbalimbali kutokana na kuwa na utofauti wa ha...

MBUNGE MULUGO AKABIDHI PIKIPIKI KWA WATENDAJI WA KATA TATU, ASEMA ZITASAIDIA KURAHISISHA UKUSANYAJI MAPATO.

Image
Na Ibrahim Yassin,Songwe  Mbunge wa Jimbo la Songwe, Mhe. Philipo Mulugo (Papaa) amekabidhi pikipiki kwa watendaji wa kata tatu za Halmashauri ya Wilaya ya Songwe ili ziweze kuwasaidia watendaji hao kurahisisha kutimiza majukumu yao. Amesema moja ya kitendea kazi muhimu katika ukusanyaji mapato ya halmashauri ni pikipiki ambazo zitamrahisishia kufika maeneo mbalimbali kwa wakati kukusanya mapato. Amesema wilaya ya Songwe ni moja ya wilaya yenye masoko mengi ya minada hivyo pikipiki hizi zitafanikisha mtendaji kufika kwa wakati na kutimiza majukumu yake. Mbunge Mulugo amekabidhi pikipiki hizo leo Jumanne Agosti 27, 2024 kwa watendaji wa Kata za Mwambani, Kanga na Udinde ambazo ni kata ziliz okuwa zimebaki kukamilisha kata zote 18 kupata pikipiki. Naye mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wlaya hiyo  Secilia Kavishe amesema anaipongeza serikali ya awamu ya sita kuona umuhimu wa kutoa pikipiki kwenye kata zote 18 hali itakayorahisisha shughuri za kiutendaji kwa maafisa hao. Akimuwakilish...

NANYARO AHAMASISHA UPANDAJI MITI WAZEE WA MILA WAKIADHIMISHA SIKU YAO YA UPENDO.

Image
Na Ibrahim Yassin.Songwe  MJUMBE wa halmashauri kuu CCM mkoa wa Songwe Ombeni Nanyaro amemuomba mkuu wa wilaya ya Momba Elias Mwandobo kuuenzi mwenge wa uhuru kwa kuhamasisha kila kaya kupanda miti na kutunza mazingira. Nanyaro ameyasema hayo jana katika sherehe  zilizowakutanisha pamoja kati ya  viongozi wa chama na serikali na viongozi wa mila kujadili mambo mbalimbali ikiwemo mmomonyoko wa maadili kwa jamii. Maadhimisho ya siku ya wazee wa mila yalifanyika wilayani Momba mkoani humo ambapo viongozi wa chama na  serikali walionekana kuunga mkono jitihada za wazee hao kusaidia ulinzi wa nchi kwa kukemea mabaya. Alisema ipo haja ya kuuenzi mwenge wa uhuru kwa kuhamasisha upandaji wa miti kuepuka uharibifu wa mazingira,kujihadhari na mabadiriko ya tabia nchi ikiwemo kudhibiti ukataji miti ovyo. "Mkuu wa wilaya hamasa ifanyike kwa kila kaya ipande japo mti mmoja  kwani itasaidia kudhibiti mabadiliko ya tabia nchi na hata wanaoharubu mazingira kwa kukata miti wadhibitiwe. Nae chifu M...

DC ITUNDA AKUTANA NA UONGOZI WA KAMPUNI YA MAMBA INAYOWEKEZA KWENYE UCHIMBAJI WA MADINI ADIMU DUNIANI RARE EARTH METALS ENEO LA NGWALA.

Image
Na Ibrahim Yassin.Songwe  Mkuu wa Wilaya ya Songwe Solomon Itunda jana amefanya kikao na uongozi wa Kampuni ya Mamba Minerals inayowekeza katika uchimbaji wa madini adimu duniani ya Rare Earth Metals kijiji cha Ngwala Wilayani Songwe. Kikao hicho ambacho pia kimehudhuriwa na Katibu Tawala wa Wilaya ya Songwe, Godfrey Kawacha kimefanyika katika ofisi za Mkuu wa Wilaya zilizopo Mkwajuni makao makuu ya wilaya. Akizungumza baada ya Kikao hicho, Mhe. Itunda amesema kuwa uongozi huo umemweleza maendeleo ya mchakato wa tathmini na mipango ya kuanza kulipa fidia kwa wananchi ambao maeneo yao yalichukuliwa kupisha mradi. Mkuu huyo wa Wilaya ameusisitiza uongozi huo kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kwa kila hatua wanayofikia ili wananchi wajue kinachoendelea katika eneo hilo. Pia, DC Itunda amesema kuwa uongozi huo umemweleza kuwa ujenzi wa mgodi huo utaanza Januari, 2025. "Tumefanya kikao na wenzetu wa Mamba, Kampuni ambayo inayowekeza katika uchimbaji wa madini adimu duniani ya Rare Ear...

Kukamilika kwa daraja la mto Mwalisi kutachagiza ukuaji wa uchumi

Image
Na Ibrahim Yassin,Songwe WANANCHI wa vijiji vya Lupeta , Mwalisi na Lema wameishukuru serikali inayoongozwa na Rais Dkt,Samia Suluhu Hassan kupitia Serikali chini ya Shirika la Taifa la Madini STAMICO kwa kurahisisha mawasiliano na kuwanusurua na vifo vitakanavyo na ajali za kusombwa na maji mto Mwalisi. Daraja la mto Mwalisi ni moja ya Daraja hatari mkoani humo lililosababisha kuwepo kwa hatari mbalimbali ikiwemo watu kuliwa na mambo huku wajawazito wakijifungulia njiani wakishindwa kuvuka hasa nyakati za mvua za masika. Serikali za awamu zote ziliahidi kujenga Daraja kubwa bila mafanikio huku wananchi wakiendelea kuhatarisha Maisha yao kwa kuvuka kwenye kivuko cha mianzi kilichosababisha baadhi kutumbukia na kuliwa na mamba miaka ya nyuma. Baada ya kukamilisha ujenzi wa daraja linalounganisha Wilaya za Rungwe na Kyela Mkoa Mbeya na Wilaya ya Ileje,Mbozi Mkoani Songwe,wananchi wametoa ya moyoni wakipongeza serikali kwa kusikia kilio kilichodumu tangu nchi hii ipate uhuru. Wakizungumza...

Mwenyekiti serikali ya Mtaa auawa kikatili akutwa kwenye ukuta wa shule

Image
Na Ibrahim Yassin.Songwe ALIYEKUWA mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Hewe kijiji cha Itepula wilayani Mbozi mkoani Songwe, Jamson Mwakitalima Mtafya (59) amekutwa ameuawa kisha mwili wake kutupwa kwenye ukuta wa shule ya msingi Ndyuda akitokea benki kutoa fedha. Akizungumza leo August 22/2024 jirani wa marehemu huyo, Assa Kamwela alisema marehemu jana aliaga nyumbani kwake kuwa anaenda benki kutoa hela majira ya asubuhi lakini hakurudi hadi majira ya mchana alipokutwa pembezoni mwa ukuta wa shule ya msingi Nyuda akiwa amekufa. Alisema marehemu hakuwa na ugomvi na mtu kwani aliwahi kuwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa miaka 5 iliyopita na alikuwa mshauri mzuri kwenye jamii katika masuala mbalimbali. Mwenyekiti wa kijiji cha Itepula Bonifasi Mkisi alisema marehemu alitoka nyumbani kwake jana saa moja asubuhi kwenda Mlowo kutoa fedha akiwa na usafiri wa pikipiki lakini siku hiyo hakurudi hadi walipomkuta kauawa na kutupwa kwenye uzio wa shule ya Ndyuda. Alisema tukio hilo ni muendelezo wa ...

POLISI SONGWE WAPIGWA MSASA KUELEKEA UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA

Image
Na Ibrahim Yassin.Songwe Mkuu wa kitengo cha kampuni binafsi za ulinzi na Polisi Wasaidizi kutoka makao makuu ya Jeshi la Polisi Dodoma, kamisheni ya Polisi jamii Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Ulrich Matei akiwa na viongozi wengine kutoka makao makuu ya polisi Dodoma wametoa elimu na mafunzo kwa askari mkoani Songwe. Kamishna Matei akiambatana na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Paul Sanga kutoka Kamisheni ya Operesheni na Mafunzo Agosti 21, 2024 wamefanya ziara ya kikazi Mkoani Songwe na kutoa elimu kuhusu mambo mbalimbali yakiwemo maandalizi ya uchaguzi. DCP Matei aliwaelekeza askari kutambua wajibu wao katika uchaguzi na kutojihusisha na itikadi za kisiasa bali kutenda haki bila ya kujali itikadi za Vyama vya kisiasa, Dini, Jinsia au Kabila. Kikoa hicho kilifanyika ukumbi wa Polisi Vwawa Wilaya ya Mbozi na kuudhuriwa na Jeshi la Mage reza, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Idara ya uhamiaji na Jeshi la Akiba (Mgambo). Katika semina hiyo jeshi la polisi pia walishiriki ma...

Tozo za chanjo za mifugo zazua balaa Songwe

Image
Na Ibrahim Yassin,Songwe WANANCHI jamii ya wafugaji kutoka bonde la Kamsamba wilayani Momba mkoani Songwe wamezikusanya risiti walizopewa baada ya kutozwa tozo za chanjo ya mifugo zilizoandikwa majina ya mikoa ya Katavi na Kigoma jiji huku wakitaka ufafanuzi. Wananchi hao jana wamekusanya risiti hizo na kuzikabidhi kwenye mkutano wa hadhara ulioitishwa na mdau wa maendeleo na mkulima bora wa bonde hilo Abdul Ntila uliolenga kutoa elinu ya uelewa kwa wakulima kupinga wanasiasa kugeuka daraja la kuwanyonya kupitia stakabadhi gharani kwa zao la ufuta. Awali akizungumza kwenye mkutano huo Sakala Sinkala mkazi wa Mpapa alisema wapo kwenye zoezi la kuchanja mifugo yao na wanapolipa fedha wanapewa risiti zenye majina ya mkoa wa Katavi na Kigoma jiji hivyo wanaomba sababu kwani ni bora ziandikwe jina la Momba ama mkoa wa Songwe. Nae Samwel Silumbwe mkazi wa Mkonko alisema katika bonde hilo kuna wafugaji wengi, kima cha chini kaya moja inakuwa na ng"ombe 200 na wao wamekubali kuchanja la...

WAZAZI WANAOWATUMIA WATOTO KWENYE BIASHARA MUDA WA SHULE WAONYWA

Image
Na Israel Mwaisaka,Nkasi Afisa Ustawi wa jamii wilayani Nkasi mkoani Rukwa Oscar Mdenye amewaonya Wazazi wanaowatumia Watoto wao kufanya biashara za kuuza miwa katika stand kuu ya Namanyere muda ambao walitakiwa wawepo shule. Onyo Hilo limekuja baada ya kubainika kuwepo Kwa Watoto ambao ni Wanafunzi muda wa kuwepo shule wakiwa wameambatana na Wazazi wao kwenye biashara mbalimbali mjini Namanyere ikiwemo biashara ya miwa na Watoto hao kukosa haki Yao ya kupata elimu. Sambamba na Hilo afisa Ustawi huyo amewaonya wamiliki wa vibanda vya kuchezesha Magame kwenye Computer kutoruhusu Watoto kucheza michezo hiyo muda wa shule na kuwa atakayebainika atachukuliwa hatua Kali za kisheria. Amefafanua kuwa hivi Sasa imebainika Watoto wengi majira ya asubuhi ukimbilia kujificha kwenye michezo hiyo ya Game na kutokwenda shule na wakati mwingine ulazimika kuiba fedha za Wazazi wao na kwenda kucheza michezo hiyo. Amedai kuwa kumekuwepo na malalamiko mengi kutoka Kwa Wazazi juu ya Watoto wao ambao wengi...

Familia yadhamilia kumuona Rais Ikulu kupigania haki waliyopokwa na kanisa

Image
Na Ibrahim Yassin,Songwe FAMILIA ya Mwambande Kalinga (50) mkazi wa mtaa wa Mantengo 'B' kata ya Vwawa wilayani Mbozi mkoani Songwe, inajiandaa kwenda Ikulu Chamwino jijini Dodoma kumuona Rais Dkt, Samia kutoa dukuduku lao. Kalinga amemwambia Mwandishi wa habari hizi jana kuwa ameamua kwenda Ikulu kumuona Rais baada ya kanisa la Moravian usharika wa Vwawa kubomoa nyumba zake 2 na kufyeka mazao kwa madai kuwa eneo hilo ni la kwao. Mbali na kubomolewa nyumba 2.pia mazao mbalimbali iliwemo miti na kahawa anadai ilifyekwa huku akiachwa akiishi kwa shida na familia yake. No Alisema miaka ya nyuma eneo hilo lenye hekali 700 lilikuwa likitumika na muwekezaji ambaye ni Mzungu alipoondoka walikuja wawekezaji wengine na baadae akaja mzee Zebedayo Chungu aliyekaa eneo hilo kama muwekezaji. Anasema baada ya Mzee Chungu kukaa hapo alimgawia baba yake hekari 12 wakiwemo watu wengine ambao walijenga nyumba za kuishi huku sehemu nyingine wakifanya shughuri za kilimo. Anasema baada ya baba yak...

Siku chache baada ya mahakama kuu kumpa ushindi Mjane Mariamu wadau wapongeza hukumu hiyo

Image
                  MAKALA MJANE MARIAM BAADA YA KUSHINDA KESI AELEZA MAGUMU ANAYOPITIA KATIKA ARDHI ALIYOACHIWA NA MUMEWE. Na Mwandishi wetu,Songwe SIKU chache baada ya mahakama ya Rufaa Kanda ya Mbeya kumpa ushindi Mjane Mariam Kalupande kuwa ndiye mmiliki halali wa eneo gombaniwa kati yake na mtoto wa shemeji yake aitwaye Rozina Kalupande lililopo kijiji cha Haraka kata ya Ezya wilayani Mbozi wadau waeleza kukoshwa na hukumu hiyo. Kesi hiyo namba 64/2023 ya Rufaa ilifunguliwa katika mahakama kuu kanda ya Mbeya na Taasisi ya wakina mama Foundation, Kijiji cha Haraka na halmashauri ya Mbozi baada ya awali Mariamu Kalupande (MJANE) kuwafungulia kesi katika baraza la ardhi kwa kuvamiwa eneo lake. Mzee mmoja aitwaye Isaka Mtafya mkazi wa Mbozi alisema amepong eza hukumu hiyo akisema eneo hilo ni la Leston Kalupande huku akisikitisha kitendo cha mjane Mariamu kufanyiwa ukatili kwenye eneo la famiia yake. HISTORIA YA MZEE KALUPANDE. Madai ya Familia ya Kalupande dhidi ya Wakina mama na watot...