Posts

Showing posts from May, 2024

NAUWASA wautambulisha mradi wa maji wa Mil.815

Image
Na Israel Mwaisaka,Rukwa MAMLAKA ya maji mjini Namanyere NAUWASA imeutambulisha rasmi mradi wa upanuzi na uboreshaji wa maji Namanyere wenye thamani ya Tshs,mil.815 Akiutambulisha mradi huo kaimu mkurugenzi mtendaji NAUWASA Hamisi Honero amesema kuwa mradi huo umekwisha anza kutekeleza baada ya mchakato wa kuwapata wazabuni mbalimbali wa kutekeleza mradi huo kuwapatikana. Amedai kuwa katika kiasi hicho cha fedha cha mil.815 wao mpaka sasa wameshapata Tshs,Mil.700 na kuwa milioni 115 iliyobaki itaingia wakati wowote huku mradi huo ukiendelea kutekelezwa. Honero amesema kuwa katika mradi huo kuna shughuli nyingi zinatarajia kufanyika ambazo ni kujenga tank lenye ujazo wa lita 100.000 litakalokuwa juu ya mnara wa mita 9,kujenga nyumba 5 za mitambo katika maeneo ya Mabatini,Misunkumilo,Majengo na Nakambili. Kazi nyingingine ni ujenzi wa Chemba,uchimbaji wa visima vitatu,ununuzi wa mabomba yenye urefu wa km 15 kata zote,ununuzi wa pump 5,utafiti wa maji chini ya ardhi,usafishaji na upimaji...

TAG Nkasi yakabidhi mifuko 10 ya sementi kwa mkuu wa wilaya ili kukarabati shule

Image
Na Israel Mwaisaka,Nkasi SERIKALI wilayani Nkasi imelishukuru kanisa la Assemblies of God (TAG) la mjini Namanyere kwa msaada wa mifuko 10 ya Cementi iliyoitoa kwa ajili ya kuikarabati shule ya msingi Nkomolo ambayo inaitaji ukarabati mkubwa baada ya shule hiyo kuchakaa sana. Shukrani hizo zimetolewa na mkuu wa wilaya Nkasi Peter Lijualikali kwenye maadhimisho ya miaka 85 ya TAG toka kuanzishwa kwake Nchini na miaka 36 toka lianzishwe Namanyere baada ya kanisa hilo kuyatumia maadhimisho hayo kuchangia ukarabati wa shule hiyo kwa kutoa mifuko hiyo ya Sementi. Amesema kuwa serikali ipo bega kwa bega na taasisi za dini katika kuhakikisha Maisha ya jamii yanaboreshwa na kuwa kitendo cha kanisa kuunga mkono jitihada za wananchi katika kujiletea maendeleo ni jambo la busara na la kuigwa na taasisi nyingine ikiwa ni pamoja na watu binafsi. Hivyo ameutaka uongozi wa shule na Kijiji cha Nkomolo kuhakikisha kuwa sementi hiyo inatumika sawa katika kukarabati shule na kazi yake ionekane na kuwa ku...

MADAKTARI BINGWA WAPOKELEWA NKASI KWA BASHASHA

Image
Na Israel Mwaisaka,Nkasi WANANCHI wilayani Nkasi Mkoani Rukwa wamewapokea Madaktari bingwa Kwa bashasha Huku wakihaidi kuwapatia ushirikiano wa kutosha katika kipindi chote watakachokuwepo wilayani humo. Akizungumza wakati wa mapokezi ya Madaktari hao Kaimu Mganga mkuu wa wilaya Josepha Joseph amesema kuwa ujio wa Madaktari .hao ni utekelezaji wa programme ya Rais jamuhuri ya muungano wa Tanzania DK,Samia Suluhu Hassan hivyo ni muhimu Kwa Wananchi hao kuitumia fursa hiyo vizuri. Amesema kuwa Madaktari hao watano watakuwepo wilayani Nkasi Kwa muda wa siku Tano na wapo watano wakiwa wamebobea katika nyanja mbalimbali kama Vile katika magonjwa ya Kina Mama na Wajawazito,magonjwa ya Watoto,upasuaji,usingizi na magonjwa ya ndani kama Presha na kisukari. Kaimu mkurugenzi mtendaji halmashauri ya wilaya Ladislaus Mzelela Kwa upande wake amewataka Wananchi wote kuhakikisha watu wote wenye shida za kiafya kuitumia vizuri fursa hiyo na kuahidi wa kama halmashauri kuwapatia ushirikiano wa hari n...

Afisa wa Benki NMB Nkasi afariki kwa kujinyonga

Image
Na Israel Mwaisaka,Nkasi MFANYAKAZI wa Benki ya NMB tawi la Nkasi katika wilaya Nkasi mkoani Rukwa John Maduhu (32) mkazi wa Majengo mjini Namanyere amekutwa amekufa nyumbani kwake kwa kujinyonga kwa kamba. Akizungumzia tukio hilo mwenyekiti wa mtaa wa Majengo soko kuu William Katutu alisema kuwa tukio hilo limegundulika jana asubuhi ya Mei 10,2024 majira ya saa 3 asubuhi na wafanyakazi wa benki hiyo baada ya mfanyakazi mwenzao kutoonekana ofisini asubuhi. Alisema kuwa tukio hilo liligundulika baada ya kuchungulia dirishani katika nyumba aliyokuwa akiishi marehemu ndipo walipouona mwili ukining’inia kwenye mlango wa chumbani kwake katika nyumba aliyokuwa akiishi. Mwenyekiti huyo wa mtaa amedai kuwa baada ya hilo walitoa taarifa Polisi ambao walivunja mlango na kuingia ndani na kumkuta marehemu akiwa amejining’iniza juu ya mlango wa chumbani kwa kutumia kamba ya jiko la umeme. Afisa mtendaji wa mtaa huo wa Majengo Flora Mbaule amekiri kutokea kwa tukio hilo na kuwa katika vipimo vili...

RUWASA YATAKIWA KUVILINDA VYANZO VYA MAJI

Image
Na Israel Mwaisaka,Nkasi MKUU wa wilaya Nkasi Peter Lijualikali amewaagiza Wakala wa maji na usafi wa mazingira vijijini RUWASA kuhakikisha wanavilinda vyanzo vya maji kwa kuzuia watu kulima karibu na vyanzo vya maji ikiwa ni pamoja na kupanda miti ili kulinda hifadhi hizo Maagizo hayo ameyatoa leo alipokuwa akitembelea na kukagua miradi ya maji ambapo ameweza kutembelea mradi wa maji Kabwe, Matala,Kirando na Mkinga ambapo amesema kuwa vyanzo vyote vya maji inabidi vilindwe ipasavyo na kuhakikisha shughuli mbalimbali za kibindamu zinafanywa mbali na vyanzo hivyo. Amesema kuwa ili miradi hiyo iweze kudumu na kuleta tija kwa jamii ni lazima itunzwe kisheria ili jamii iweze kupata maji wakati wote na kuondoa tatizo la maji katika jamii kama ilivyo ndoto yam he,Rais ya kumtua ndoo Mama kichwani . Akitoa taarifa kwa mkuu wa wilaya kaimu meneja wa RUWASA wilayani Nkasi Jaffari Amri amesema kuwa miradi mitatu ya maji ya Kabwe,Kirando na Mkinga imepata changamoto baada ya maji ya ziwa Tanga...

JMAT- VIONGOZI WA DINI WASIKUBALI KUTUMIWA NA WANASIASA

Image
Na Israel Mwaisaka,Rukwa VIONGOZI wa Dini wilayani Nkasi mkoani Rukwa wametakiwa kusimama imara na kutoruhusu kuyumbishwa na Wanasiasa katika kipindi hiki tunachoelekea kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu mwakani. Wito huo umetolewa leo na mwenyekiti wa jumuia ya maridhiano na amani Tanzania (JMAT) wilaya Nkasi Hadhiri Daruweshi alipokuwa akizungumza kwenye kikao cha jumuia hiyo ambapo amedai kuwa viongozi wa dini wakiyumba wanaweza kuwatoa nje ya mstari waumini wao na kubaki na sintofahamu. Amesema kuwa wao kama viongozi wa dini jukumu lao kubwa katika kipindi hiki kuelekea katika chaguzi hizo kubwa ni kujikita zaidi katika kuhubiri amani na upendo kwa nguvu zote kwani kwa kufanya hivyo kutasaidia kuwepo kwa amani katika taifa hili. Hadhiri amedai kuwa kwa uzoefu katika maeneo mbalimbali duniani ambako viongozi wa dini wamechanganya siasa na dini ni lazima kuwepo kwa machafuko na kunakotokana na kutoweka kwa amani katika  jamii hiyo. Awali katibu wa jumuia hiyo Mchun...