WADAU WATOA YA MOYONI WAKIKOSHWA NA MIRADI YA RUWASA NA TARULA-RAIS SAMIA-RAS SENEDA WATAJWA.
Na Ibrahim Yassin,Songwe SIKU chache baada ya mwenge wa uhuru kufika na kukagua miradi ya maendeleo hususani miradi muhimu ya miundombinu ya barabara na madaraja na ile ya maji,wananchi wametoa ya moyoni baada ya miradi hiyo kumkosha mkimbiza mwenge kitaifa. Mkoa wa Songwe ni moja ya mikoa mipya nchini uliomegwa kutoka mkoa wa Mbeya Octoba 18/2015 ikiwa na wilaya 4 na halmashauri 5 yaani Ileje,Momba,Tunduma,Mbozi na Songwe na wilaya 4 ambazo ni Momba,Songwe,Ileje na wilaya mama ya Mbozi. Mkoa una kata 94,vijiji 307 huku ikiwa na wakazi 1.344,687 kati ya hao wanaume ni 643,679 wanawake ni 701,008 ambapo idadi kubwa ya wakazi ni wakulima na wafugaji,hii ni kwa mujibu wa sense ya watu na makazi. Kwa mwaka 2022/23 Rais Dkt,Samia alitoa Tsh,Bilioni 20.9 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya barabara,na mwaka 2023/2024 alitoa Bilioni 17, Kwa upande wa miradi ya maji Rais Dkt,Samia mwaka 2023/24 baada ya kutoa fedha wakala ulipanga kutekeleza jumla ya miradi 1,546 katika mikoa 25 nchini ikiw...