Posts

Showing posts from August, 2025

ZAIDI YA BILIONI 4.8 ZATOLEWA KWA WAKAZI 494 KUPISHA MRADI WA KISASA.

Image
Na Ibrahim Yassin,Songwe WANANCHI zaidi ya 494 wilayani Mbozi mkoani Songwe wameanza kupokea fedha kwa ajili ya malipo ya fidia ya kupisha mradi wa kitaifa wa kituo cha ukaguzi wa pamoja (Iboya). Asilimia 70 ya bidhaa  zinazovushwa bandari ya Dar es salaam zinapita kwenye mpaka wa Tunduma,ujenzi wa ikiwemo  njia nne zitahepusha msongamano wa magari naajari na kuongeza tija za kiuchumi. Akizungumza leo Agost 31/ 2025 Meneja wa wakala wa barabara mijini na vijijini (Tanroads) mkoani Songwe Mhandisi Suleiman Bishanga amesema wapo kuwapatia cheki za malipo wananchi kupisha mradi. Anasema kabla ya kuwapatia malipo hayo serikali ilifanya tathimini kwa kuwashirikisha wenyeji wa maeneo hayo ambapo kila mlengwa analipwa kutokana na ukubwa wa eneo husika. Amesema eneo hilo la Iboya patajengwa mradi mkubwa wa kitaifa cha kisasa cha ukaguzi wa magari yaendayo katika nchi za kusini mwa afrika (Sadc) itakaoendana na njia nne inayotarajiwa kujengwa. ''Lengo la serikali ni kujenga barabara ya ...

MKULIMA WA ZAO LA MIHOGO AJITOLEA KUJENGA SHULE INAYOONGOZA KITAIFA KUSAIDIA WENYE UHITAJI.

Image
MAKALA ‘’Mimi nilisomeshwa na Padri Lyaunga wa kanisa la Katoliki kwa sasa ni marehemu alizikwa Lupa tinga tinga,nikaanza kulima hekari 70 nilipopata fedha nikaanza kujenga shule iitwayo Save Life inayoongoza Kitaifa kusaidia wenye uhitaji’’. Na Ibrahim Yassin,Mbeya JAMII Nchini yaaswa kujikita katika kusaidia jamii yenye uhitaji hasa katika sekta ya elimu na kilimo ili iondokane na lindi la umasikini na kujikwamua kiuchumi. Lupi Charles Mwaipalu ni mkazi wa kijiji cha Kandete Kata ya Itope wilayani Kyela mkoani Mbeya,ni mkulima wa zao la mihogo aliyekuwa  mfano wa kuigwa kwa kujenga shule ya darasa la awali hadi darasa la saba kusaidia wenye uhitaji.. Wakulima wengi wa Kyela wamekuwa wa hawalipi kipaumbele zao hilo wengi wao wamejikita katika zao la mpunga na Kakao ambao kwa sasa wameanza kujifunza uzoefu kwa mkulima huyo. Mwandishi wa Makala hii,alifika katika kijiji hicho iliyopo shule ya Save Life (Saidia Maisha) kuzungumza na mkurugenzi huyo ambaye alitoa historia yake kuwa aliso...

BIL 6.830.ZA RAIS DKT SAMIA ZATUMIKA KUJENGA VITUO VYA KUTOLEA TIBA NA UNUNUZI WA VIFAA.

Image
MAKALA ‘’serikali ya awamu ya sita umeondoa vifo vya mama na mtoto,kwa kujenga zahanati kila kijiji,kituo cha afya kila kata na hospital ya wilaya,awali tulitibiwa kwa waganga wa kienyeji na wakunga wa jadi,wengi walipoteza maisha hasa watoto baada ya kuzaliwa’’ Na Ibrahim Yassin,Songwe MAELFU ya wakazi wa wilaya ya Songwe mkoani hapa,hasa wajawazito waliokuwa wakitegemea kuzalishwa na wakunga wa jadi wamepata matumaini mapya baada ya serikali kujenga hospitali ya kisasa ikiwa na vifaa tiba. Wilaya ya Songwe ni moja ya wilaya 5 mkoa wa Songwe yenye post kodi namba 54100, Katika sensa ya mwaka 2022 wakazi walihesabiwa 229,219 . Katika wilaya ya Songwe maeneo maarufu ni Mkwajuni ambako ndio makao makuu ya wilaya. Saza ni eneo maarufu kwa uchimbaji madini na kuna mgodi mkubwa wa Shanta Gold Mine, Kanga na Mbangala. Ilianzishwa mwaka 2015 ikiwa imepakana na wilaya ya Momba mkoani hapa na Milele mkoani Katavi upande wa chini na upande wa chini imepakana na wilaya ya Sumbawanga mkoani Rukwa ...

BIL 6.830.ZA RAIS DKT SAMIA ZATUMIKA KUJENGA VITUO VYA KUTOLEA TIBA NA UNUNUZI WA VIFAA.

Image
‘’serikali ya awamu ya sita umeondoa vifo vya mama na mtoto,kwa kujenga zahanati kila kijiji,kituo cha afya kila kata na hospital ya wilaya,awali tulitibiwa kwa waganga wa kienyeji na wakunga wa jadi,wengi walipoteza maisha hasa watoto baada ya kuzaliwa’’ Na Ibrahim Yassin,Songwe MAELFU ya wakazi wa wilaya ya Songwe mkoani hapa,hasa wajawazito waliokuwa wakitegemea kuzalishwa na wakunga wa jadi wamepata matumaini mapya baada ya serikali kujenga hospitali ya kisasa ikiwa na vifaa tiba. Wilaya ya Songwe ni moja ya wilaya 5 mkoa wa Songwe yenye post kodi namba 54100, Katika sensa ya mwaka 2022 wakazi walihesabiwa 229,219   . Katika wilaya ya Songwe maeneo maarufu ni Mkwajuni ambako ndio makao makuu ya wilaya. Saza ni eneo maarufu kwa uchimbaji madini na kuna mgodi mkubwa wa Shanta Gold Mine, Kanga na Mbangala. Ilianzishwa mwaka 2015 ikiwa imepakana na wilaya ya Momba mkoani hapa na Milele mkoani Katavi upande wa chini na upande wa chini imepakana na wilaya ya Sumbawanga mkoani Rukwa Wabun...

WAKANDARASI WANAWAKE WAZAWA WAPEWA ANGALIZO KUKAMILISHA MIRADI KWA WAKATI.

Image
Na Ibrahim Yassin,Songwe SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi imetoa rai kwa Makampuni 15 ya Makandarasi Wanawake waliopata fursa ya ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami yenye urefu wa kilometa 20 katika barabara ya Ruanda - Idiwili Mkoani Songwe kuutekeleza mradi huo ipasavyo kwa ubora, uaminifu na muda uliopangwa. Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Barabara kutoka Wizara ya Ujenzi Mhandisi Alois Matei wakati akimwakilisha Katibu Mkuu Balozi Mhandisi Aisha Amour katika ufunguzi wa Kongamano la Tano la Makandarasi Wanawake lililofanyika siku za hivi karibuni jijini Dar Es salaam. “Mafanikio ya mradi huu wa barabara ambao mmepewa na Serikali wa majaribio utafungua milango kwa miradi mingine zaidi ili Makandarasi  Wanawake wengine pia wapate fursa hizo”, amesisitiza Mhandisi Matei. Ameongeza kuwa Serikali imepanua wigo wa thamani ya miradi inayotolewa kwa Makandarasi Wazawa hadi kufikia Bilioni 50 ikiwa ni hatua muhimu ya kuweza kushiriki miradi mikubwa ya maendeleo inayoendelea hapa nchin...

WAZIRI WA ULINZI NA JKT AFUNGA MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA MKOA MWANZA

Image
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mheshimiwa Dkt. Stergomena Lawrence Tax (Mb) tarehe 15 Agosti 2025, amehitimisha kwa kufunga Mafunzo ya Jeshi la Akiba Mkoa Mwanza, shughuli iliyofanyika katika viwanja vya Mwanankanda wilayani Magu. Akitoa hotuba yake wakati wa Ufungaji Mafunzo hayo, Dkt. Tax amewataka wahitimu hao kutumia vizuri maarifa na weledi walioupata katika mafunzo hayo ili kukidhi matarajio ya Taifa na malengo ya misingi ya majukumu ya Jeshi la Akiba. Aidha, amewataka kudumisha nidhamu, Uzalendo na Uhodari katika utekelezaji wa majukumu yao huku wakifahamu kwamba Jeshi la Akiba ni sehemu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.  

ASILIMIA 80 YA WANANCHI KUTUMIA NISHATI SAFI YA KUPIKIA IFIKAPO 2034 KATAVI

Image
  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe, Shamimu Mwariko amesema kutokana na jitihada zinazoendelea kuchukuliwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia (2024-2034) ni dhahiri kwamba lengo la 80% ya wananchi kutumia nishati hiyo litafikiwa ifikapo Mwaka 2034. Amesema hayo Agosti 15, 2025 wakati wa kutambulisha mradi wa kusambaza majiko ya gesi ya kilo 6 na vichomeo vyake kwa bei ya ruzuku ya shilingi 19,500 kwa jiko unaoratibiwa na REA na kutekelezwa na Mtoa huduma Kampuni ya Taifa Gas Limited iliyoshinda zabuni ya kutekeleza mradi huo katika Mkoa wa Katavi. Alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa kinara wa kampeni ya Nishati Safi ya Kupikia kwa kuhakikisha kwamba Tanzania inaningia, inasimamia na inaishi katika mazingira ya Nishati Safi. Alibainisha kuwa Halmashauri ya Mpimbwe tayari imeanza uhamasishaji wa matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia k...

KAEGELE NA KAZUKAMWE WAIBUKA KIDEDEA KURA ZA MAONI CCM WILAYANI NKASI

Image
Na Israel Mwaisaka, Nkasi ‎ ‎Salum Kazukamwe na Moses Kaegele wameshinda katika Kura za maoni za kuwania Ubunge katika Majimbo mawili ya Nkasi Kaskazini na kusini yanayounda wilaya Nkasi ‎ ‎Akitoa taarifa juu ya zoezi zima la upigaji wa Kura za maoni lililofanyika Jana katibu wa CCM wilaya Nkasi Anastazia Almasi amesema kuwa wilaya Nkasi inaundwa na Majimbo mawili ya Uchaguzi na makada 10 wa CCM walifanikiwa kuingia katika kinyang'anyiro hicho na wawili hao kupenya kuweza kupeperusha bendera ya CCM kwenye uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba 29,2025.. ‎ ‎Amesema kuwa kwa upande wa Jimbo la Nkasi Kaskazini Salumu Kazukamwe ameshinda kwa kupata Kura 2956 akifuatiwa na John Sichilima aliyepata kura 1471, Jonas Kifunda 560, Thomas Kalunga kura 320 na wa mwisho Ni David Siame aliyeambulia 137. ‎ ‎Kwa upande wa Jimbo la Nkasi kusini Moses Kaegele ameshinda kwa kupata Kura 3028 akifuatiwa na Vicent Mbogo aliyepata 1,623, Evarist Christopher Mwanansao Kura 465,Desderius Mipata Ku...

BIL 6.830.ZA RAIS DKT SAMIA ZATUMIKA KUJENGA VITUO VYA KUTOLEA TIBA NA UNUNUZI WA VIFAA.

Image
‘’serikali ya awamu ya sita umeondoa vifo vya mama na mtoto,kwa kujenga zahanati kila kijiji,kituo cha afya kila kata na hospital ya wilaya,awali tulitibiwa kwa waganga wa kienyeji na wakunga wa jadi,wengi walipoteza maisha hasa watoto baada ya kuzaliwa’’ Na Ibrahim Yassin,Songwe MAELFU ya wakazi wa wilaya ya Songwe mkoani hapa,hasa wajawazito waliokuwa wakitegemea kuzalishwa na wakunga wa jadi wamepata matumaini mapya baada ya serikali kujenga hospitali ya kisasa ikiwa na vifaa tiba. Wilaya ya Songwe ni moja ya wilaya 5 mkoa wa Songwe yenye post kodi namba 54100, Katika sensa ya mwaka 2022 wakazi walihesabiwa 229,219   . Katika wilaya ya Songwe maeneo maarufu ni Mkwajuni ambako ndio makao makuu ya wilaya. Saza ni eneo maarufu kwa uchimbaji madini na kuna mgodi mkubwa wa Shanta Gold Mine, Kanga na Mbangala. Ilianzishwa mwaka 2015 ikiwa imepakana na wilaya ya Momba mkoani hapa na Milele mkoani Katavi upande wa chini na upande wa chini imepakana na wilaya ya Sumbawanga mkoani Rukwa Wabun...

VITENDO VYA UKATILI KWA WANAWAKE NA WATOTO VYAPUNGUA NKASI

Image
‎ Na Israel Mwaisaka,Nkasi ‎ ‎Uwepo wa maafisa maendeleo ya jamii ngazi ya kata,kamati za kupambana na ukatili na uwepo wa asasi za kiraia katika maeneo mengi kumesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza vitendo vya ukatili katika jamii. ‎ ‎Hayo yamebainika Jana kupitia vikao vya MTAKUWWA vilivyoketi katika kata za Majengo, Kirando na Isale vilivyofadhiliwa na shirika lisilokuwa la kiserikali Kituo Cha sheria na ustawi wa jamii Namanyere (SHEUJANA) katika KUPATA tathimini juu ukatili kati ya Wanawake na Watoto. ‎ ‎Katika vikao hivyo ilibainika kuwa vitendo vya ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto vimekua vikipungua kwa kiasi kikubwa na kuwa Hilo limetokana na uwepo wa maafisa maendeleo ya jamii katika kata nyingi sambamba na ushiriki mkubwa wa asasi za kiraia baada ya jamii kupata elimu ya kutosha juu ya ubaya was vitendo vya ukatili unaotokea katika jamii. Mkurugenzi wa shirika la Kituo Cha sheria na Ustawi wa jamii Namanyere Godfrey Ntangare amedai kuwa kulingana na mila na desturi za jam...