Mvua yaleta maafa nyumba 30 zaezuliwa 150 wakosa makazi
Na Israel Mwaisaka, Kalambo JUMLA ya watu 150 wamebaki bila makazi baada ya nyumba 30 kuezuliwa paa na nyingine zimebomoka kufuatia mvua kubwa iliyonyesha juzi katika Kijiji cha Kaluko kata ya Chitete wilayani Kalambo mkoani Rukwa. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi jana Mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho, Edwin Kasama alisema kuwa mvua hiyo ilianza kunyesha Siku ya Octoba 26 majira ya saa 10 jioni zikiwa zimeambatana na upepo mkali. Alisema kuwa ulianza upepo mkali Kisha ikafuatia mvua kubwa ambapo ilisababisha kubomoka baadhi ya nyumba kijijini hapo huku nyumba nyingine zikiezuliwa mapaa na kuziacha baadhi ya familia bila nyumba za kuishi. "Baadhi ya wanakijiji nyumba zao zimebomoka kabisa hawana hata sehemu ya kulala tena wana watoto hivyo tunaiomba serikali iwasaidie kwakua wanapitia wakati mgumu kwakua vitu vyao vimeharibika kabisa" alisema Kasama. Mmoja wa wakazi wa Kijiji hicho Paskalia Katata alisema kuwa tukio hilo limewaacha katika hali mbaya kwani hawana f...