WACHUNGAJI NA VIONGOZI WA DINI WATAKIWA KUFANYA KAZI KUEPUKA KUWA OMBAOMBA.
Na Abraham Mwaitenda, Songwe IMEELEZWA kuwa viongozi wa dini wakiwemo wachungaji wa makanisa wametakiwa kufanya kazi za kujiingizia kipato ili kujikwamua kiuchumi kuondokana na uombaomba. Kauli hiyo imetolewa jana .na mmoja wa wadhamini wa kanisa la Marafiki Duniani Mch.,Erick Roy .raia wa Marekani wakati akizungumza na viongozi wa kanisa la.Friend Church mjini Tunduma. Mch. Roy amesema kufanya kazi ni Ibada hivyo wachungaji na viongozi wengine wametakiwa kufanya kazi na kuwawezesha waumini wao mbinu za kutafuta mali ili wajikwamue kiuchumi. Amesema Mungu mwenyewe alifanya kazi siku 6 lakini alipumzika siku ya 7 na akasisitiza kuwa asiyefanya kazi na asile ,hivyo ni wajibu watumishi wa mungu kufanya kazi ili kujiingizia kipato. Amesema wachungaji wakiwa na uchumi mzuri wataendesha ibada vizuri, waumini wakiwa.na uchumi watahudhuria ibada na kutoa sadaka na fungu la kumi vizuri na kanisa litaemdelea. " wachungaji wengi wamekuwa wakiendesha maisha kwa kutegemea sadaka za waumini ...