Mvua yenye upepo mkali yasababisha maafa nyumba zabomoka, familia zakosa makazi
Na Israel Mwaisaka, Nkasi Nyumba 29 zimebomoka na nyingine kuezuliwa para kufuatia mvua yenye upepo mkali katika vijiji vya Mabatini na Mkangale kata ya Namanyere huku familia kadhaa zikiachwa bila ya makazi. Diwani wa kata ya Namanyere Nestory Kaloto akitoa taarifa mbele ya kamati ya maafa ya wilaya ikiongozwa na mkuu wa wilaya Nkasi Peter Lijualikali amesema kuwa tukio Hilo limetokea juzi jioni baada ya mvua iliyokuwa imeambatana na upepo mkali kunyesha na kusababisha maafa hayo. Amesema kuwa wengi wao wanahifadhiwa na majirani zao na kuwa wengi wanahitaji msaada mkubwa na wa haraka Ili kuweza kurudia katika hari Yao ya kawaida. Mkuu wa wilaya ambaye pia ndiye mwenyekiti wa kamati ya maafa ya wilaya Peter Lijualikali kwa upande wake amewataka wakazi wa eneo Hilo kupanda miti ya kutosha Ili kukabiliana na changamoto hiyo Na kuwa ameagiza halmashauri kupeleka mara Moja Miche ya miti mbalimbali Ili waanze kuipanda miti hiyo. Pia amewataka kufuata kanuni za ujenzi pale wanapoanza kujen...