WAANDIKISHAJI WAPIGA KURA WATAKIWA KUFANYA KAZI YAO KWA UWELEDI ILI KUFANIKISHA JUKUMU HILO LA KITAIFA
Na Israel Mwaisaka,Nkasi WASHIRIKI wa mafunzo ya uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura awamu ya pili wametakiwa kufanya kazi yao kwa ueledi mkubwa ili kuweza kufanikisha jukumu hilo la msingi la kitaifa na kuhakikisha wale wote wenye sifa wanajiandikisha katika daftari hilo. Wito huo umetolewa jana na afisa mwandikishaji wa wilaya Nkasi Ladislaus Mzelela alipokuwa akifunga mafunzo ya siku moja kwa maafisa Waandikishaji wasaidizi na waendesha vifaa ambapo amedai kuwa jukumu lao ni kubwa hivyo uweledi pekee utapelekea kufanikisha kazi hiyo kwa ufanisi. Alisema kuwa mafunzo hayo waliyoyapata kwa njia ya nadharia na vitendo yalijikita katika ujazaji fomu mbalimbali zitakazotumika vituoni fomu za kiapo cha kutunza siri na kujitoa uanachama katika chama cha siasa ikiwa ni pamoja na namna ya kuandikisha wapiga kura wapya,wanaorekebisha au kuboresha taarifa zao ikiwa ni pamoja na wale wanaoondolewa au kufutwa kwenye daftari la kudumu la mpiga kura. Hivyo amewataka kutambua uz...