Posts

Showing posts from December, 2024

UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA JANUARI 12 MKOANI RUKWA

Image
Na Israel Mwaisaka,Rukwa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imetangaza ratiba ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwenye mikoa ya Rukwa, Njombe, Songwe na Ruvuma ambapo zoezi hilo litafanyika kwa siku saba kuanzia tarehe 12 hadi 18 Januari, 2025. Hayo yameanishwa kwenye hotuba ya Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Mhe. Jacobs Mwambegele iliyosomwa kwa niaba yake kwenye mikutano ya Tume na wadau wa uchaguzi iliyofanyika leo tarehe 31 Desemba, 2024 kwenye mikoa ya Rukwa, Njombe, Songwe na Ruvuma. Mhe. Mwambegele ambaye aliwakilishwa na wakurugenzi mbalimbali wa Tume kwenye mikutano hiyo, amesema mikoa hiyo itafanya uboreshaji kwenye mzunguko wa tisa na kwamba tayari Tume imekamilisha uboreshaji kwenye mikoa 19 ambayo ilijumuisha mizunguko nane kati ya mizunguko 13 ambayo imepangwa kukabilisha zoezi hilo nchini. “Leo tupo hapa Rukwa na wenzetu wapo kwenye mikoa ya Njombe, Ruvuma na Songwe ikiwa ni maandalizi ya uboreshaji wa Daftari kwenye m...

MCHIMBAJI MDOGO ATOA AJIRA AKIUNGA JITIHADA ZA SERIKALI,ATOA PENDEKEZO.

Image
                          MAKALA wachimbaji wadogo watoa mapendekezo namna serikali inavyoweza kuongeza kipato kupitia sekta ya madini Na,  Ibrahim yassin,chunya yassin.ibrahimu@yahoo.com  0718382817. Mchimbaji mdogo wa madini ya dhahabu katika halmashauri ya wilaya ya chunya mkoani mbeya,khamis salum kindai ametoa ajira kwa vijana zaidi ya 100 kutoka mikoa mbalimbali huku akitoa mapendekezo kwa serikali namna ya kuongeza tija ya uzalishaji ikiwemo kuondoa changamoto zilizopo kwa wachimbaji. sekta ya madini ni moja ya chanzo muhimu ambacho kinaingiza mapato makubwa na kuwatajirisha watu huku serikali ikitegemea mapato kutokana na tozo kutoka katika sekta hiyo. ikiwa sekta hiyo ni muhimu ambapo serikali ikiweka mikakati mizuri kuongeza mapato iangazie kufanya maboresho kwa wachimbaji ikiwa ni pamoja na kuwapatia mikopo pamoja na maeneo ya uchimbaji kwani kwa sasa wengi wao wamekuwa wakichimba kwenye maeneo yenye leseni za watu licha ya kuwa maeneo hayo hawayatumii. akizungumza na gazeti...

UHARIBIFU WA MAZINGIRA BONDE LA ZIWA RUKWA LAHITAJI SEKTA NNE KUNUSURU.

Image
                                          MAKALA Na Ibrahim Yassin,Songwe yassin.ibrahimu@yahoo.com   0766936392. KUKITHIRI kwa uharibifu wa mazingira kwenye vyanzo vya maji katika bonde la ziwa Rukwa kunahitaji ushirikiano wa zaidi ya sekta tatu kudhibiti, limebainika. Uharibifu huo wa mazingira unafanywa hasa na wafugaji na wachimbaji madini ya dhahabu ambao baadhi yao wamekuwa wakitililisha maji yenye kemikali kwenye mito na wengine wakikata miti ovyo na kuharibu uoto wa asili. Baada ya mwandishi wa habari hizi kupata taarifa za uharibifu huo,ulifanyika uchunguzi katika bonde la ziwa Rukwa imebainika kuwa sekta zaidi ya tatu zinahitajika ili kunusulu.  Imebainika kuwa uharibifu mkubwa unaofanywa na wachimbaji wa dhahabu katika Bonde hilo unahatarisha kutoweka kwa miti ya asili pamoja na uoto wa asili kwenye vyanzo vya Maji. Mwandishi alifika  katika vyanzo vya mito ya Lupa, Tete, Zila, Kipoka, Mbuzi, Kalungu, Saza, Lwika, Kilinga na Mto Mlamba Ng'ombe ambako shughuli za uchimbaj...

Serikali yamkana Mwalimu aliyewasimamisha Wanafunzi na kuwa siyo maelekekezo ya serikali

Image
Na Israel Mwaisaka,Nkasi HALMASHAURI ya wilaya Nkasi mkoani Rukwa imetoa ufafanuzi juu ya tukio la Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Izinga tarafa ya Wapembe Legiucy Martin Kawimbe anayedaiwa kuwafukuza shule Wanafunzi 9 kuwa hayo hayakua maelekezo ya serikali bali ni mgogoro kati ya Walimu na Wazazi uliojitokeza Kijijini hapo uliopelekea Mwalimu mkuu kuwasimamisha shule na kuwataka Wazazi wao wawatafutie shule nyingine na kuwa alienda kinyume na utaratibu na Wanafunzi hao wamerejeshwa shule na hatua za kinidhamu zitachukuliwa pindi uchunguzi unaoendelea utakapokamilika. Akitoa ufafanuzi juu ya hilo mbele ya Waandishi wa habari mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya Nkasi Afraha Hassan amesema kuwa Mapema Leo Kuna taarifa iliyokuwa ikisambaa kwenye mitandao ya kijamii juu ya Mwalimu mkuu wa shule hiyo ya Izinga kuwafukuza Wanafunzi 9 kama ni maelekezo ya serikali na kuwa baada ya kulifuatilia Kwa kina suala Hilo walibaini kuwa Mwalimu huyo aliwasimamisha shule Watoto hao baada ya k...

Wadau wa mapambano dhidi ya Ukimwi walalamikia Comdomu ya kike kutumika kinyume cha utaratibu

Image
Na Israel Mwaisaka, Rukwa WADAU wa mapambano dhidi ya ugonjwa wa Ukimwi wilayani Nkasi mkoani Rukwa wamedai kuwa kondomu ya kike haitumiki ipasavyo kiasi kwamba Kwa Sasa chuma kilichopo kwenye kondomu hiyo utumika kama bangiri Kwa baadhi ya Wanawake. Akizungumza kwenye Maadhimisho ya siku ya Ukimwi Jana mratibu wa asasi ya SEELS Neoni Sanga lidai kuwa licha ya mbinu mbalimbali za kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa wa Ukimwi kuendelea kutumia pia Condomu ya kike ni Moja ya nyenzo muhimu sana katika mapambano hayo lakini imekuwa haitumiki ipasavyo ambapo Kwa Sasa chuma chake kilichopo katika Condomu hiyo utumika kama bangiri za za kuvaa mikononi . Alidai kuwa katika tafiti walizozifanya wamegundua kuwa Wanawake wengi bangiri walizonazo ni chuma kilichokuwa kwenye Condomu hiyo ya kike na kuiomba jamii kuacha kuvaa bangiri hizo Bali Condomu hiyo ya kike itumike sawasawa kwenye matumizi yake katika harakati muhimu za kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa wa Ukimwi. Pia alisema kuwa Kwa Sas...