Posts

Showing posts from December, 2023

BIBI MJANE AMUANGUKIA RAIS DR,SAMIA KUPOKWA MALI ALIZOACHIWA NA MUMEWE IKIWEMO HEKARI 31 ZA ARDHI.

Image
MAKALA APANGA KWENDA IKULU KUONANA NA RAIS DR,SAMIA KUELEZA ANAVYONYANYASIKA JUU YA MALI ALIZOACHIWA NA MUMEWE mjane Mariam Kalupande akizungumza na mwandishi wa habari jinsi ardhi yake inavyotaka kuporwa. Na Israel Mwaisaka WAKATI serikali ya awamu ya sita ikiongozwa na Rais Dr,Samia Suluhu Hassan ikiwaagiza viongozi ngazi zote kuhakikisha inamaliza migogoro ya ardhi nchini,hali hiyo imekuwa tofauti kwa wilaya ya Mbozi mkoani Songwe ambako bibi mjane ananyanyasika juu ardhi zake. Ardhi inathamani kubwa katika kuendeleza maisha ya binadamu ambayo inatumika kwa kujenga nyu mba za biashara ,viwanda,Taasisi ,makazi na kuendesha shughuli za kilimo kwa mazao ya biashara na chakula hivyo endapo inatokea migogoro inaweza  kuzuka mapigano na kuhatarisha uhai wa watu. Hali hiyo imeikumba familia ya mzee Leston Kalupande aliyeanzisha taasisi ya kusaidia jamii ambaye kwa sasa ni marehemu ,baada ya kifo chake kumezuaka mgogoro mzito ambapo mdogo wake anadaiwa kunyang’anya mali za taasisi na sasa y...

Mradi mkubwa wa maji kuanza kujengwa Kalambo

Image
Na Baraka Lusajo,Kalambo – Rukwa Mhandisi Marwa webiro – kaimu meneja wa Ruwasa wilayani Kalambo Serikali kupitia wakala wa maji safi na usafi wa mazingira ruwasa imeanza ujenzi wa mradi mkubwa wa bwawa la maji wenye thamani ya shilingi billioni 1,770,686,091.83 utakao hudumia zaidi ya vijiji 5 na watu elfu kumi na mbili (12000) katika kata ya mbuluma wilayani Kalambo mkoani Rukwa. Akiongea wakati wa ukaguzi wa mradi wa bwawa hilo kaimu meneja wa ruwasa wilayani humo mhandisi Marwa Webiro amesema mradi huo utahusisha ujenzi wa tuta la bwawa na ujenzi wa utoro wa maji mita 368 na kusema mpaka sasa kazi zilizo fanyika ni pamoja na usafishaji wa eneo sambamba na upimaji wa alama za tuta lenye urefu wa mita 368 na pimaji wa mita za mianguko ya maji. Kamati ya siasa ya chama cha mapinduzi ccm wilayani humo imefanya ukaguzi wa mradi huo ambapo mkuu wa wilaya ya Kalambo Lazaro Komba  amesema mradi huo utahudumia vijiji 5 vyenye idadi ya watu 12000 kwa gharama ya shilingi billion moja 1,770,...

Wafanyabiashara za minadani waonywa kupanda malori na mizigo kulinda usalama wao

Image
Na Israel Mwaisaka,Nkasi KAMANDA wa Polisi mkoani Rukwa Shadrack Masija amewataka Wafanyabiashara za minadani kuacha mara Moja kupanda magari ya mizigo wanapokwenda kwenye biashara zao Bali wajitenganishe na mizigo kwa kupanda mabasi ya abiria. Akizungumza na Wananchi wa wilaya Nkasi Leo chini ya Programme ya Polisi jamii kupitia mazoezi ya utimamu (Jogging) amesema kuwa kumekuwepo na utamaduni wa Wafanyabiashara wa kupanda magari ya mizigo kwenda minadani na kuwa wengi wamefariki au kujeruhiwa inapotokea ajali na kuwa sasa iwe mwisho kufanya hivyo na kinachotakiwa sasa ni kuisafirisha mizigo kwenye maloli na wao wasafiri kwenye mabasi ya abiria kufuata mizigo Yao. Alisema kuwa ni kosa kubwa kwa Wafanyabiashara kuchanganyana na mizigo kwenye maloli na kuwa maelekezo yalikwishatolewa kwa viongozi wao na kuwa atakayeendelea kupanda kwenye mabasi atakua anakaidi maagizo halali ya serikali na kuwa hayo yanalenga kuwafanya Wafanyabiashara wanakua salama wakati wote kutokana na umuhimu wao k...

Wafanyabiashara wa minadani waonywa kupanda malori bali wapande mabasi ya abiria

Image
Na Israel Mwaisaka,Nkasi KAMANDA wa Polisi mkoani Rukwa Shadrack Masija amewataka Wafanyabiashara za minadani kuacha mara Moja kupanda magari ya mizigo wanapokwenda kwenye biashara zao Bali wajitenganishe na mizigo kwa kupanda mabasi ya abiria. Akizungumza na Wananchi wa wilaya Nkasi Leo chini ya Programme ya Polisi jamii kupitia mazoezi ya utimamu (Jogging) amesema kuwa kumekuwepo na utamaduni wa Wafanyabiashara wa kupanda magari ya mizigo kwenda minadani na kuwa wengi wamefariki au kujeruhiwa inapotokea ajali na kuwa sasa iwe mwisho kufanya hivyo na kinachotakiwa sasa ni kuisafirisha mizigo kwenye maloli na wao wasafiri kwenye mabasi ya abiria kufuata mizigo Yao. Alisema kuwa ni kosa kubwa kwa Wafanyabiashara kuchanganyana na mizigo kwenye maloli na kuwa maelekezo yalikwishatolewa kwa viongozi wao na kuwa atakayeendelea kupanda kwenye mabasi atakua anakaidi maagizo halali ya serikali na kuwa hayo yanalenga kuwafanya Wafanyabiashara wanakua salama wakati wote kutokana na umuhimu wao k...

Watakaokwamisha Watoto kuandikishwa darasa la awali na msingi kukiona

Image
Na Israel Mwaisaka, Sumbawanga SERIKALI wilayani Nkasi Mkoani Rukwa imewaonya watendaji wa idara ya elimu kutoweka vikwazo vitakavyo sababisha baadhi ya watoto waliofikia umri wa kuanza elimu ya awali na darasa la kwanza wakakosa fursa hiyo. Mkuu wa wilaya hiyo, Peter Lijualikali alitoa agizo hilo jana wakati akitoa taarifa kwa waandishi wa habari katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya mkuu wa mkoa, juu ya mafanikio ya utekelezaji wa miradi katika sekta ya Elimu, Afya na Maji ambapo alisema kuwa miradi yote imekamilika kwa zaidi ya asilimia 95. Alisema kuwa hivi sasa ni wakati wa kuandikisha watakao anza elimu ya awali na shule ya msingi hivyo hataki kusikia mtoto yoyote ameshindwa kuanza shule kwasababu ya michango ama cheti cha kuzaliwa kwani kunataarifa zisizo rasmi kuwa mtoto atakae kosa cheti hicho hata andikishwa shule. "Natoa Onyo kwa walimu wakuu na watendaji wengine wa elimu kutodai michango yoyote kwa mzazi anaye mwandikisha shule mtoto wake kwani serikali imeshajenga mad...
Image
Na Israel Mwaisaka, Sumbawanga SERIKALI wilayani Nkasi Mkoani Rukwa imewaonya watendaji wa idara ya elimu kutoweka vikwazo vitakavyo sababisha baadhi ya watoto waliofikia umri wa kuanza elimu ya awali na darasa la kwanza wakakosa fursa hiyo. Mkuu wa wilaya hiyo, Peter Lijualikali alitoa agizo hilo jana wakati akitoa taarifa kwa waandishi wa habari katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya mkuu wa mkoa, juu ya mafanikio ya utekelezaji wa miradi katika sekta ya Elimu, Afya na Maji ambapo alisema kuwa miradi yote imekamilika kwa zaidi ya asilimia 95. Alisema kuwa hivi sasa ni wakati wa kuandikisha watakao anza elimu ya awali na shule ya msingi hivyo hataki kusikia mtoto yoyote ameshindwa kuanza shule kwasababu ya michango ama cheti cha kuzaliwa kwani kunataarifa zisizo rasmi kuwa mtoto atakae kosa cheti hicho hata andikishwa shule. "Natoa Onyo kwa walimu wakuu na watendaji wengine wa elimu kutodai michango yoyote kwa mzazi anaye mwandikisha shule mtoto wake kwani serikali imeshajenga mad...

DC NKASI AWA MBOGO KWA WAVAMIZI WA HIFADHI YA MFILI AWATAKA WAONDOKE HARAKA

Image
Na Israel Mwaisaka,Nkasi MKUU wa wilaya Nkasi mkoani Rukwa Peter Lijualikali amewapiga marufuku watu waliovamia na kulima kwenye hifadhi ya msitu wa Mfili ambacho pia ni chanzo cha maji na kuwa yeyote atakayekutwa ndani ya hifadhi hiyo atachukuliwa hatua kali za kisheria. Agizo hilo amelitoa jana alipokuwa akizungumza na Wananchi wa eneo hilo na kusema kuwa serikali ilishatoa maagizo ya mtu yeyote asiingie ndani ya hifadhi hiyo ya Mfili na kufanya shughuli zozote za kiuchumi lakini ameshangaa kuona kwamba bado kuna watu wameingia ndani ya hifadhi hiyo na kulima. Hivyo amesema kuwa kuanzia sasa ni marufuku kuingia ndani ya hifadhi hiyo ya msitu na kwa wale waliolima ndani ya hifadhi hiyo wahesabu kwamba wameingia hasara kwa maana hairuhusiwi kabisa kuingia ndani ya hifadhi hiyo na kuendelea na shughuli za kilimo. ""Ni marufuku kabisa kuendelea na shughuli ndani ya hifadhi hiyo na kwa wale waliolima wamefanya kosa na wamevunja sheria na kwa maana hiyo hesabuni hasara kwani sit...

DC NKASI AWA MBOGO KWA WAVAMIZI WA HIFADHI YA MFILI AWATAKA WAONDOKE

Image
Na Israel Mwaisaka,Nkasi MKUU wa wilaya Nkasi mkoani Rukwa Peter Lijualikali amewapiga marufuku watu waliovamia na kulima kwenye hifadhi ya msitu wa Mfili ambacho pia ni chanzo cha maji na kuwa yeyote atakayekutwa ndani ya hifadhi hiyo atachukuliwa hatua kali za kisheria. Agizo hilo amelitoa jana alipokuwa akizungumza na Wananchi wa eneo hilo na kusema kuwa serikali ilishatoa maagizo ya mtu yeyote asiingie ndani ya hifadhi hiyo ya Mfili na kufanya shughuli zozote za kiuchumi lakini ameshangaa kuona kwamba bado kuna watu wameingia ndani ya hifadhi hiyo na kulima. Hivyo amesema kuwa kuanzia sasa ni marufuku kuingia ndani ya hifadhi hiyo ya msitu na kwa wale waliolima ndani ya hifadhi hiyo wahesabu kwamba wameingia hasara kwa maana hairuhusiwi kabisa kuingia ndani ya hifadhi hiyo na kuendelea na shughuli za kilimo. ""Ni marufuku kabisa kuendelea na shughuli ndani ya hifadhi hiyo na kwa wale waliolima wamefanya kosa na wamevunja sheria na kwa maana hiyo hesabuni hasara kwani sit...

Waganga wafawidhi wa vituo vya kutolea huduma za afya wasaini mkataba wa uwajibikaji

Image
Na Israel Mwaisaka,Rukwa MGANGA mkuu wa mkoa Rukwa Ibrahimu Isaac amewataka waganga wafawidhi wa vituo vya kutolea huduma za afya kusimamia utoro kazini ikiwa ni pamoja na ulinzi wa vifaa tiba katika vituo vyao ikiwa ni pamoja na kufunga CCTV Camera kwenye vituo vyenye mali nyingi ili kulinda mali hizo za serikali. Akizungumza na Waganga Wafawidhi wa vituo vya kutolea huduma za afya wilayani Nkasi katika ukumbi wa mkurugenzi mtendaji wa wilaya amesema kumekuwepo na utoro wa reja reja kazini ambapo hata vituo katika baadhi ya maeneo uchelewa kufunguliwa na kusisitiza utunzaji wa vifaa tiba maana kumeibuka wimbi wa wizi wa vifaa tiba katika maeneo mbalimbali Nchini. Alisema Wananchi wanazihitaji sana huduma za afya hivyo ni lazima zitolewe kwa weredi mkubwa na kuhakikisha miundo mbinu iliyowekwa na serikali inatumika vizuri katika kuboresha huduma za afya katika vituo wanavyofanyia kazi. Pia amewataka Waganga hao wafawidhi kuwa wabunifu katika utoaji wa huduma kwa kuongeza kutoa huduma ...

Elimu ya Ukimwi yasaidia kupunguza maambukizi mapya ya Ukimwi

Image
Na Israel Mwaisaka,Nkasi KUFUATIA elimu inayotolewa na Wataalamu wa afya juu ya kukabiliana na ugonjwa wa Ukimwi wilayani Nkasi mkoani Rukwa imepelekea maambukizi mapya kupungua baada ya watu wengi kujitokeza kupima na kujua hari zao na kuchukua hatua za haraka pale wanapobainika kuwa na Virus hivyo. Katika taarifa iliyotolewa na mratibu wa Ukimwi wilayani Nkasi Lucas Mhigi kwenye maadhimisho ya siku ya Ukimwi jana ni kuwa kasi kubwa ya watu wanaojitokeza kupima afya ni kubwa na kurahisisha mapambano ya kukabiliana na ugonjwa huo ikiwa ni pamoja na kuhakikisha Waathirika wazitumia vyema dawa za kufubaza Virusi vya Ukimwi . Alisema kuwa katika kufikia malengo ya 95 tatu ,lengo la kwanza ni upimaji wa VVU ambapo wamefanikiwa kufikia asilimia 98,Matumizi ya dawa wamefikia asilimia 98.3 na lengo la mwisho ni la upungufu wa Virus mwilini kufikia asilimia 97. Jumla ya Wananchi 29,668,wamejitokeza kupima ikiwa Wanawake ni 15,748 na Wanaume 13,920 kwa mwaka 2021/2022 waliokutwa na maambuk...