Watendaji kata na vijiji waaswa kusimamia amani
Na Israel Mwaisaka,Nkasi Mkuu wa wilaya ya Nkasi Mkoani Rukwa Peter Lijualikali amewataka Maafisa watendaji kata na vijiji kuhakikisha wanasimamia suala Zima la amani katika maeneo yao ili wananchi waendelee kufanya kazi na kujiletea maendeleo. Akizungumza kwenye kikao kilichowajumuisha watendaji hao na viongozi wa kamati ya ulinzi na usalama wa wa wilaya kwenye ukumbi wa Mkurugenzi Mtendaji wa wilaya November 28, 2025, amesema kuwa wao kama viongozi, moja ya jukumu lao kubwa ni kuhakikisha suala zima la amani na utulivu linakuwepo katika maeneo yao, ikiwa ni pamoja na kusimama miradi yote ya maendeleo inayotekelezwa katika kata na vijiiji vyao. Amedai kuwa hivi karibuni Waziri Mkuu Dk.Mwigulu Lameck Nchemba, alitoa agizo la Kila mtumishi wa Umma kuwajibika katika nafasi yake hivyo wao kama watendaji wanalo jukumu la kuhakikisha kuwajibikaji kwa watumishi wanaowaongoza unakuwepo. Aidha Mkuu huyo wa wilaya amewataka watendaji hao kuwatumia watu maarufu katika maeneo yao wakiwemo wazee ...