Skauti waadhimisha kuzaliwa kwa mwanzilishi wa Skauti duniani kwa kupanda miti na matendo ya huruma
Na Israel Mwaisaka,Rukwa Katika kuadhimisha kumbukizi ya kuzaliwa kwa mwanzilishi wa Skauti duniani Sir Roberth Barden Powell Skauti mkoa Rukwa wameiazimisha siku hiyo kwa kupanda miti na kufanya matendo ya huruma katika hospitali ya Wilaya Nkasi. Akiongoza zoezi hilo Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya Nkasi ambaye pia Afisa uhamiaji wa Wilaya Nkasi Mrakibu mwandamizi Aloyce Fuko alisifu Wazo hilo kwani linaenda sambamba na matamanio ya Rais Dkt,Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha tunakabiliana na mabadiliko ya tabia Nchi kwa kupanda miti. Alisema kuwa kutokana na shughuli nyingi za kibinadamu miti mingi imekua ikikatwa na kutuweka katika mazingira hatarishi yanayotokana na uharibifu huo wa mazingira na kuwa kitendo Cha Skauti Cha kuja na Wazo hilo katika kukumbuka mwanzilishi wa Skauti duniani ni kulitendea haki taifa. Awali kamishina wa Skauti mkoa Rukwa Hassan Kikoloma alisema kuwa licha ya zoezi hilo la kupanda miti pia watawatembelea wagonjwa wa hospitali ya wilaya Nkasi na ...