Wafungwa jela maisha kwa kosa la ubakaji
Na Israel Mwaisaka, Nkasi MAHAKAMA ya wilaya Nkasi Mkoani Rukwa imemhukumu kifungo Cha maisha jela Kelvin Pungama (23) mkazi wa Kijiji Cha Karundi Kwa kosa la kumbaka mtoto wa miaka Minne wa darasa la awali katika shule ya msingi Fyengerezya. Akitoa hukumu hiyo leo hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya wilaya Nkasi Adamu Mwanjokolo amesema anamtia hatiani mtuhumiwa chini ya kifungu Cha sheria (130) na (2) (e) na 131 (1) na (3) Cha kanuni ya adhabu sura ya 16 marejeo ya mwaka 2022 ni baada ya mahakama kuridhishwa na maelezo na ushahidi uliotolewa upande wa jamuhuri pasipo kuacha shaka yoyote Awali upande wa mashitaka ukiongozwa na Waendesha mashitaka wa serikali Irene Mwabeza na Cedric Mashauri waliieleza mahakama hiyo kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo Septemba 5,2023 katika Kijiji Cha Karundi ambapo mtoto huyo alikwenda kumsalimia Dada yake na wakati wakiwa shambani alimuacha mtoto huyo nyumbani na ndipo kijana huyo alipomshika na kumpeleka chumbani kwake na kuanza kumbaka. Waendesha ...