KATIBU MKUU UMOJA WA SHULE ZA SEKONDARI NCHINI ACHUKUA FOMU YA UBUNGE.
''Kugombea ni haki ya kila mtanzania,hivyo nimetia nia ya ubunge kuomba ridhaa kwa chama,nina malengo makubwa ya kuipaisha Mbozi kiuchumi,kuweka mikakati endelevu kwenye zao la Kahawa'' Na Ibrahim Yassin, Songwe Katibu mkuu wa Umoja wa wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania Bara na kada lia lia wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Frank Ndile amechukua fomu ya kuomba kuteuliwa na Chama hicho kugombea nafasi ya ubunge Jimbo la Mbozi Mkoani Songwe. Ndile leo June 29,2025 amefika katika ofisi za chama hicho zilizopo wilaya ni Mbozi Mji wa Vwawa mkoani hapa na kukabidhiwa fomu na katibu wa chama hicho wilaya ya Mbozi Julius Mbwiga. Ndile ambaye pia ni meneja wa shule za sekondari Kanan amesema amewiwa kuchukua fomu kugombea ubunge Jimbo la Mbozi kwa lengo la kuwatumikia wananchi ikiwepo kutatua chagamoto zilizopo. katibu wa ccm wilayani Mbozi yenye majimbo mawili Julius Mbwaga akimkabidhi fomu ya kugombea Frank Ndile aliyevaa kofia.katika ofisi za ccm wilayani humo. Alizitaja changam...