Posts

Showing posts from April, 2024

RC CHONGOLO APONGEZA UKUSANYAJI MAPATO TRA ILEJE AKIPOKEA CHANGAMOTO.

Image
Na Ibrahimu Yassin,Songwe Serikali imeombwa kukipandisha hadhi kituo cha forodha cha Isongole wilayani Ileje Mkoani Songwe kutoka daraja C kwenda B pamoja na ujenzi wa majengo yenye hadhi mpakani....anaripoti Ibrahim Yassin,Songwe Leo Aprili 28/2024 Afisa mfawidhi kituo cha forodha Isongole katika mpaka wa Tanzania na Malawi Charles Chacha.baada ya mkuu wa Mkoa huo Daniel Chongolo kukaguana kupokea taarifa ya shughuli zinazotekelezwa mpakani hapo. Chacha amesema kutokana na kituo hicho kutokuwa na hadhi ,kwa sasa kinafanya kazi kama pacha na kituo cha forodha chaTunduma mpakani mwa Tanzania na Zambia  Chacha amesema serikali inatakiwa kukipandisha hadhi kituo hicho kimekidhi vigezo vya kuongeza wigo wa ukusabyaji mapato kutoka Sh 7.8 milioni mwaka 2019 mpaka kufikia zaidi ya Sh 400 mwaka 2024 licha ya mpaka huo kuwa na vipenyo vinavyopelekea mapato mengi kupotea. Amesema mpaka huo unapitisha bidhaa mbalimbali zinazoingia na kutoka ikiwepo, zao la Mahindi, Soya, Karanga, vinywaji, saruj...

WATOTO 32,168 NKASI KUPATIWA CHANJO YA SARATANI YA SHINGO YA UZAZA (HPV)

Image
Na Israel Mwaisaka,Rukwa WILAYA ya Nkasi mkoani Rukwa inatarajia kuwachanja Watoto wa kike wapatao 32,168 kukabiliana na maradhi ya ugonjwa wa saratani ya shingo ya uzazi Akizindua chanjo hiyo katika shule ya msingi ya Isunta kaimu mkuu wa wilaya ya Nkasi na ambaye pia ni mkuu wa wilaya Kalambo Razaro Komba amewataka wanananchi kuhamasika na kuhakikisha watoto wao wote waliofikisha umri wa miaka 9 hadi 14 wanaipata chanjo hiyo. Alidai kuwa zoezi hilo la chanjo ambalo litadumu kwa muda wa siku 5 litakua na maana sana kama walengwa wote wataipata chanjo hiyo ili kuweza kukabiliana na ugonjwa huo wa saratani ya shingo ya uzazi ambalo kwa sasa limekuwa ni tatizo kubwa na limeleta athari katika jamii. Mkuu huyo wa wilaya amefafanua kuwa chanjo hiyo imeanza kutolewa toka mwaka 2014 mkoani Kilimanjaro na mpaka sasa imedumu kwa muda wa miaka 8 na serikali imeendelea kuitoa chanjo hiyo kutokana na changamoto wanayoipata Wanawake hasa pale wanapokumbwa na ugonjwa huo. Hivyo mkuu huyo wa ...

MATUMIZI YASIYO SAHIHI YA VIUATILIFU YAPELEKEA MAHINDI KUKAUKA NA WAKULIMA KUPATA HASARA

Image
Na Israel Mwaisaka,Rukwa WANANCHI wa kata za Mkoe wilayani Kalambo mkoani Rukwa wameingia kwenye hari ya sintofahamu baada ya mimea yao ya Mahindi mashambani kukauka kutokana na matumizi yasiyo sahihi ya viuatilifu huku wakiiomba serikali kuwapatia elimu juu ya matumizi sahihi ya viuatilifu . Wakizungumza kwa nyakati tofauti kupitia mikutano ya hadhara Wananchi hao wamesema kuwa mazao yao mashambani hasa ya Mahindi yamekauka baada ya kutumia viuatilifu na visumbufu na kuwa ikabainika kuwa hari hiyo imetokana na matumizi yasiyo sahihi ya viuatilifu hivyo. Mmoja wa Wananchi hao Vitus Masanja alidai kuwa mazao yao mengi katika mashamba yameungua kutokana na matumizi ya viuatilifu bub hivyo kiasi cha kiwango cha mavuno kuweza kupungua katika msimu huu baada ya mahindi mengi kuungua na viuatilifu hivyo. Alisema kuwa kimsingi wao kama Wakulima wa kata hiyo wamekua wakinunua viuatilifu katika maduka mbalimbali ya pembejeo za kilimo lakini wamekuwa hawapati elimu yoyote juu ya matumizi ...

MABARAZA YA KATA YAPIGWA 'STOP'KUTOA HUKUMU YAJIKITE KWENYE USULUHISHI

Image
Na Israel Mwaisaka,Nkasi KAIMU mkuu wa wilaya Nkasi ambaye pia ni mkuu wa wilaya Kalambo mkoani Rukwa Razaro komba amepiga marufuku kwa mabaraza ya ardhi ya kata kutoa hukumu badala yake yajikite kwenye usuluhishi ili kuweza kuleta utengamano katika jamii. Agizo hilo amelitoa jana wilayani Nkasi kwenye mkutano wa Wadau kujadili mradi wa utekelezaji wa uboreshaji usalama wa milki za ardhi wilayani Nkasi ambapo amesema kuwa lengo la serikali kuanzisha mabaraza hayo lilikua ni zuri kinyume chake yamekua chanzo cha kukuza migogoro. Amesema kuwa mabaraza hayo yalipewa dhamana ya kusikiliza kesi na kutoa maamuzi lakini mwaka 2021 serikali ilibaini udhaifu kwenye mabaraza hayo na kuyaondolea nguvu ya kutoa maamuzi na badala yake yajikite kwenye usuluhishi pekee. Kufuati hari hiyo ameiagiza halmashauri ya wilaya kupitia kupitia kitengo chake cha sheria kufikia ijumaa ya wiki hii iwe imetoa mafuzo kwa wenyeviti ,makatibu na wajumbe wote wa mabaraza ya kata kuwajengea uwezo wa kisheria namna ya...

KUKAMILIKA KWA BARABARA YA KAPELE-NDARAMBO KWAWAFURAHISHA WANANCHI

Image
Na Ibrahim Yassin,Songwe. Ukarabati wa barabara ya Kakozi_Ilonga enye urefu wa kilomita 49.6 Imeelezwa kuondoa adha kwa wananchi wa kata ya Kapele na Ndalambo wilayani Momba mkoani Songwe kutumia siku 5 mpaka 7 njiani kwenda katika wa Tunduma. Ukarabati kwa barabara hiyo umekuja baada ya kupandishwa hadhi na kusimamiwa na Wakala wa Barabara Tanzania(TANROAD) Mkoa wa Songwe kutoka Wakala wa barabara za mijini na vijijini(Tarura). Wakizungumza na Mwananchi kwa nyakati tofauti leo April 3/2024 baadhi ya wananchi wamesema barabara hiyo ilikuwa kero kiuchumi lakini kwa sasa imekuwa chachu ya maendeleo kwani inawafikisha maeneo muhimu ikiwemo mji wa Tunduma.. Mkazi wa kijiji cha Kakozi Godi Mtambo , amesema awali walikuwa wanatumia siku 5 mpaka 7 kufika Tunduma kutokana na ubovu wa barabara iliyokuwa ikiasababisha magari kukwama njiani wakisaka mahitaji muhimu. "Barabara hii imekuwa mkombozi wakulima wengi wa Kata za Kapele na Ndalambo wameanza kunufaika kwa kusafirisha maza...

MCHAKATO WA KUPUMZISHA ZIWA TANGANYIKA WAKAMILIKA VIONGOZI WAPIGWA MSASA

Image
Na Israel Mwaisaka,Nkasi KAIMU mkuu wa wilaya Nkasi ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Kalambo Razaro Komba amewataka Madiwani,Viongozi wa vijiji na watumishi wote wa serikali kuhakikisha kuwa wanatoa elimu kwa wananchi katika maeneo yao juu ya hadhima ya serikali ya kutaka kulipumzisha ziwa Tanganyika kwa muda wa miezi mitatu Akizungumza kwenye kikao kilichowakutanisha madiwani na viongozi wa vijiji vilivyo katika mwambao wa ziwa Tanganyika na timu ya wataalamu kutoka wizara ya mifugo na Uvuvi amesema kuwa lengo la serikali ni kutaka kulipumzisha ziwa hilo ili kuwapa muda samaki kuweza kuzaliana na kuongeza kipato cha Wavuvi kuweza kuvua samaki wengi na wakubwa wanaostahili. Amedai kuwa kinachotakiwa ni wananchi kuuelewa mpango huo vizuri na kujua faida zitakazopatikana baada ya ziwa Tanganyika kupumzishwa kwa kipindi hicho cha miezi mitatu ikiwa ni pamoja na kila mmoja kuwa mlinzi kwa mwenzie katika kuhakikisha katika kipindi hicho cha miezi mitatu hakuna mtu atakaeingia ndani ya ziwa...

WAWILI WAFARIKI BAADA YA MLIMA KUMEGUKA NA KUFUNIKWA NA TOPE

Image
Na Israel Mwaisaka,Sumbawanga MVUA zinazoendelea kunyesha mkoani Rukwa zimesababisha kupasuka kwa kipande cha mlilima wa lyambalyamfiopa katika bonde la ziwa Rukwa wilaya ya sumbawanga na kusababisha watu wawili wa familia moja kufariki dunia katika kitongoji cha Kamoko kata ya Muze baada ya kufukiwa na tope zito lilitokana na maporoko ya maji huku nyumba 38 zikianguka katika kata ya kapenta. Wakazi wa kijiji hicho katika nyakati tofauti wamesema licha ya hilo mvua hiyo imeharibu mazao na baadhi ya nyumba kuharibiwa na watu 15 kujeruhiwa. Mganga mfawidhi wa zahanati ya kijiji cha uzia dkt maiko mwaipora amesema amewapokea watu 15 walikuwa wamejeruhiwa na watu wawili wakiwa wamefariki dunia na kuelezea hali za wagonjwa. Hata hivyo kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya hiyo imetembelea maeneo hayo, ambapo mkuu wa wilaya ya sumbawanga nyakia chirukile,amewataja waliofariki duinia kuwa ni Sai Weja ( 26) na Geshi Gwesu mwenye umri wa miaka 7 wote wakazi wa kijiji cha Uzia. Aidha amesema ...

Mbunge ashiriki kula Pasaka na Wananchi wake

Image
Na Israel Mwaisaka,Nkasi MBUNGE wa jimbo la Nkasi kusini mkoani Rukwa Vicent Mbogo ameisherehekea sikukuu ya Pasaka kwa kula pamoja na wajumbe wa mkutano mkuu wa CCM kata ya Chala pamoja na Wananchi na kuutumia muda huo kukusanya mawazo kutoka kwao ambayo atakwenda kuyapeleka bungeni. Akizungumza na viongozi hao Mbogo alidai kuwa ameamua kuwakutanisha katika sikukuu hiyo ya Pasaka ili waweze kula pamoja na kuwapa nafasi wao ya kumweleza mambo ya msingi ambayo wao wanaona kuwa yana umuhimu kwenda kuzungumzwa kwenye vikao vya Bunge la jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Alisema kuwa kuna wakati ni ngumu kwa watu kuweza kukutana na Mbunge na kumweleza mambo ya msingi na kwa kuona hilo ameamua kuitumia sikukuu ya Pasaka ili kuweza kula na kunywa pamoja na kuwa hiyo inawarahishia Wananchi kuweza kuzungumza mambo ambayo wanafikiri yanaweza kuzungumzwa na kupewa kipaumbele na mwakilishi wao katika utekelezaji Mwenyekiti wa CCM kata ya Chala Johakimu Mwakampya aliwataka Wajumbe wa mkutano huo ...