SONGWE DC -YAJIVUNIA KUKAMILISHA USAMBAZAJI UMEME NGAZI YA VIJIJI IKIKARIBIA KUKAMILISHA VITONGOJINI.
Na Ibrahim Yassin,Songwe WANANCHI katika halmashauri ya wilaya ya Songwe mkoani Songwe,wameupongeza uongozi wa shirika la umeme Tanzania (Tanesco) wilayani humo kwa kukamilisha kikamilifu usambazaji wa umeme kwenye vijiji vyote. Wilaya ya Songwe yenye vijiji 43 ikiwa na vitongoji 205 na jimbo moja la uchaguzi huku makao makuu ya wilaya yakiwa katika kata ya Mkwajuni imefikia hatua nzuri ya kukamilisha vitongoji vyote usambazaji umeme katika miezi mitatu ijao. Licha ya upya wake wilaya hiyo iliyomegwa kutoka wilaya ya Chunya mkoani Mbeya miaka kumi iliyopita ilikuwa ikikabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo uhba wa nishati ya umeme lakini katika utawala wa awamu ya sita chini ya Rais Dkt,Samia Suluhu,wamefanikiwa kusambaza umeme vijiji vyote 43. Hayo yamesemwa leo Oktoba 27/2025 na meneja wa shirika hilo wilayani Songwe Mhandisi Michael Kidoto wakati akizungumza na dira kamilifu ofisini kwake na kusema wilaya ina vijiji 43 vyote vinahuduma za umeme na sasa wamehamia kukamilisha usambazaj...