Mradi wa umeme wa TAZA kuiunganisha Afrika na Umeme
Na Israel Mwaisaka,Rukwa NAIBU waziri mkuu wa jamhuri ya mungano wa Tanzania na waziri wa nishati Dkt,Dotto Biteko ameweka jiwe jiwe la msingi njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa Kilovolti 400 kutoka Iringa hadi Sumbawanga na kuunganisha Tanzania (TAZA) pamoja na vituo vya kupoza umeme vya Tangameda,Kisada,IganjoNkangamo na Malangali. Mradi huu umelenga kuunganisha mkoa wa Rukwa na grid ya Taifa ikiwa ni pamoja na kuunganisha na mataifa mengine ya Afrika ili kuwa na umeme wa uhakika kwa asilimia 100. Akizindua mradi huo Dkt.Biteko amesema mkoa wa Rukwa haujaunganishwa na Grid ya taifa toka Nchi ipate uhuru na kuwa kutokana na jitihada mbalimbali zinazofanywa na serikali ni kutaka kuona mkoa Rukwa na mikoa mingine yote nchini Tanzania inaunganishwa kwenye gridi ya taifa ili kuwa na umeme wa uhakika na watu waweze kuutumia umeme katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo na uzalishaji mali. Alisema kuwa mradi huo ni sehemu ya maandalizi ya mwisho kwa mkoa Rukwa kuingizwa kwenye gridi...