Posts

Showing posts from September, 2023

Viongozi wa vijiji waonywa kujigeuza mahakama

Image
Na Israel Mwaisaka,Nkasi MWENYEKITI wa halmashauri ya wilaya Nkasi Pankrasi Maliyatabu amewataka viongozi wa vijijji na kata kuacha kuutumia muda mwingi kukaa ofisini na kusikiliza kesi na kuacha jukumu lao la msingi la kuhamasisha na kusimamia maendeleo na jukumu hilo la kesi wangeziachia Polisi na Mahakama. Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara katika vijijji vya Mkole na Ipanda kata ya Nkomolo amedai kuwa shughuli nyingi za maendeleo zimekuwa zikisuasua na kumbe viongozi wa vijiji na kata wamejigeuza na kuwa ni Polisi na Mahakama wakati mamlaka hizo zipo na kupelekea shughuli za maendeleo kukwama katika maeneo yao. Hilo limekuja baada ya mkazi mmoja wa kijiji cha Ipanda Michael Mhoja kumweleza mwenyekiti wa halmashauri kuwa kukwama kwa ujenzi wa zahanati kijijini hapo kumetokana na viongozi wao wa kijiji kuutumia muda mwingi kusikiliza kesi ofisini na kushindwa kabisa kusimamia shughuli za maendeleo. Kufuatia hari hiyo mwenyeki wa halmashauri aliutumia mwanya huo kuwapiga marufuku v...

Watoto  wenye  vichwa vikubwa na changamoto yakina baba kuwatelekeza

Image
Judith Ferdinand Watoto wanaozaliwa na changamoto ya ugonjwa wa kichwa kikubwa(kichwa kujaa maji kupita kawaida) na mgongo wazi nchini hapa bado ni tatizo huku moja ya sababu ikiwa ni ukosefu wa madini ya folic acid. Licha ya tatizo hilo lakini bado watoto hao wamekuwa wakikumbana na changamoto ya kunyanyapaliwa na jamii,kufichwa ndani na hata baba zao kuwatelekeza na kuwaacha wakipata malezi ya upande mmoja wa mama tu.  Hii yote ni kwa sababu bado jamii ina imani potofu juu ya ugonjwa huo wakiamini ni laana na mambo mengi.  Waandishi wa Habari wanawake Mkoa wa Mwanza wakiwa katika picha ya pamoja na watoto wenye changamoto ya kichwa kikubwa na mgongo wazi wakiwa na mama zao katika picha ya pamoja mara baada ya waandishi hao kuwatembelea kituo cha Nyumba ya Matumaini na kuwapatia msaada wa vitu mbalimbali siku ya wanawake Dunia ambayo huadhinishwa kila mwaka Machi 8. Takwimu zinaonesha kuwa katika nchi tano barani Afrika zenye watoto wengi wanaozaliwa na changamoto hiyo Tanzania ni ya ...

Saba mbaroni kwa tuhuma za udanganyifu mtihani wa darasa la 7

Image
Mwanza Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limewahoji watu saba kwa tuhuma za kosa la udanganyifu wa mtihani ya darasa la saba kwa kuwachukua wanafunzi wa sekondari na kuwafanyisha mtihani huo kwa niaba ya wanafunzi wa darasa la saba. Akizungumza jijini hapa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza SACP.Wilbord Mutafungwa, ameeleza kuwa tukio hilo lilitokea Septemba 13,2023 majira ya saa nane mchana shule ya msingi Igulumuki,Kata ya Igulumuki Tarafa ya Sengerema wakati kamati ya mitihani ya wilaya ya Sengerema ilipotembelea shule hiyo kwa ajili ukaguzi na kubaini kufanyika kwa udanganyifu huo. Ambapo mkondo namba mbili na namba tatu kulikuwa kumeingizwa wanafunzi wa sekondari watatu na kufanya mitihani ya darasa la saba. Mutafungwa amewataja watuhumiwa waliokamatwa na wanaendelea kuhojiwa ni Maiko Sheusi,(35) Mwalimu wa shule ya sekondari Sima ambaye ni msimamizi Mkuu iwa mtihani shule ya msingi Igulumuki,Musa Mwashihava (38),Mwalimu wa shule ya sekondari Kilabela ambaye ni Msimamizi wa mtihani mko...

Maaskofu wakemea mahubiri ya uongo

Image
MAASKOFU wa Kanisa la Anglikan Tanzania wamekemea chimbuko la makanisa yanayoeneza mahubiri ya uongo na kujinufaisha kupitia ongezeko la watanzania wanaodanganyika kupata mali bila kufanya kazi na changamoto zao zingine kushughulikiwa kwa haraka. Pamoja na mahubiri ya uongo, maaskofu hao wamezungumzia mmomonyoko wa maadili na anguko la mila na desturi za watanzania wakisema mambo hayo yakiachwa yaendelee taifa litaangamia. Wameyasema hayo leo kwenye kongamano lao la kitaifa la uinjilisti linalofanyika katika Chuo Kikuu Kishiriki cha Mkwawa, mjini Iringa ikiwa ni mara ya kwanza katika historia ya kanisa hilo nchini. Askofu wa Anglikan Dayosisi ya Ruaha (Iringa), Dk Joseph Mgomi alisema kanisa limewaita katika kongamano hilo wainjilisti hao kutoka nchi nzima ili wakae pamoja, kushauriana, kubadilishana uzoefu na maarifa yatakayowaweza kubadili mbinu itakayosaidia kufikisha injili ya kweli kwa wananchi. Wameyasema hayo leo kwenye kongamano lao la kitaifa la uinjilisti linalofanyika katika...

Milioni 780 kuokoa watu kuuwawa na Mamba mto Ugalla

Image
Na George Mwigulu, Nsimbo . Serikali inatekeleza ujenzi wa mradi wa maji safi na salama wenye thamani ya fedha ya Mil 780 katika Kijiji cha Katambike kata ya Ugalla Halmashauri ya Nsimbo Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi. Ujenzi wa mradi huo umeanza kutekelezwa mwenzi April mwaka huu na unatarajia kukamilika mapema mwenzi Novemba na utaokoa maisha ya watu wengi ambao vifo vyao vimeripotiwa kwa nyakati tofauti kwa sababu ya kuliwa na Mamba wakati wakichota maji katika hifadhi ya taifa ya mto Ugalla. Anna Lupembe,Mbunge wa Jimbo la Nsimbo Mkoa wa Katavi amesema hayo leo Septemba,17,2023  katika kitongoji cha Uvuvini Kijiji cha Katambike Kata ya Ugalla. Mbunge huyo amesema  kuwa kwa hatua ya ujenzi wa mradi huo upo kwenye  ujenzi wa tanki la maji lenye ukubwa wa lita Mil  za ujazo sambamba na uwekaji wa mabomba kwenye maeneo mbalimbali ya kata ya Ugalla unaendelea. ´Ninafahamu na ndio maana nikaelekeza na kuomba fedha serikali ili kuhakikisha tunapata tenki kubwa la maji hapa katika kijiji ...

Wasimamizi wa mtihani wa darasa la saba waonywa juu ya udanganyifu

Image
Na Israel Mwaisaka, Rukwa Mkuu wa wilaya ya Kalambo Mkoani Rukwa Lazaro Komba amesema Wanafunzi 7,522 kati yao wavulana wakiwa 3,404 na wasichana 4,118 wanatarajia kuanza kufanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi wilayani Kalambo na kuwaonya vikali wasimamizi watakao bainika kuvujisha mitihani na kwamba sheria kali zitachukuliwa dhidi yao. Aidha Komba amesema mitihani hiyo itafanyika kwenye vituo 330 kupitia shule 98 za wilaya hiyo na kila mkondo utakuwa na idadi ya watahiniwa 25 na kuwaonya vikali wazazi na walezi watakao bainika kujihusisha na tabia za kuwalaghai watoto wao kwa kuwazuia kufanya vizuri mitihani yao kwa nia ya kuwa ozesha na kwamba sheria kali zitachukuliwa dhidi yao Hata hivyo kwa mujibu wa afisa elimu mkoa wa Rukwa Samson Hango ,amesema idadi ya watahiniwa kwa mwaka 2023 ni 32,217 ambapo imepungua kwa jumla ya watahiniwa 1,227 sawa na asilimia 3.8% ikilinganishwa na watahiniwa 33,444 waliosajiliwa mwaka 2022. Amesema kuwa kwa upande wao kama serikali wameshafanya...

Ajira kwa watoto yafikia 'hatua hatari' huku wengi zaidi wakilazimishwa kutumikishwa - ILO

Image
Hatma ya mamilioni ya watoto iko hatarini huku wengi zaidi wakiendelea kuacha shule na kuanza kufanya kazi, mkuu wa shirika la kazi la Umoja wa Mataifa ameiambia BBC. Gilbert Houngbo, mkurugenzi mkuu wa Shirika la Kazi Duniani (ILO), alisema kumekuwa hali imeendelea kuwa "mbaya" katika maeneo yote ulimwenguni huku matatizo ya kiuchumi yakiendelea duniani. Baadhi ya aina mbaya zaidi za kazi zilihusisha unyanyasaji wa kingono. Alisema hatua za haraka zinahitaji kuchukuliwa. "Athari za Covid na kupanda kwa mfumuko wa bei na gharama ya maisha iliyofuata [na] imefanya mambo kuwa mabaya zaidi," alisema. "Labda tuchukue hatua madhubuti sasa hivi na haraka, tatizo [litaendelea] kuwa mbaya zaidi." Takwimu zilizokusanywa na Umoja wa Mataifa mapema mwaka 2020 ziligundua kuwa watoto wapatao milioni 160 walikuwa wakitumikishwa, na kwamba maendeleo ya kimataifa ya kukomesha hayo yamekwama kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 20. Bw Houngbo, waziri mkuu wa zamani ...