Siku chache baada ya mahakama kuu kumpa ushindi Mjane Mariamu wadau wapongeza hukumu hiyo


                  MAKALA

MJANE MARIAM BAADA YA KUSHINDA KESI AELEZA MAGUMU ANAYOPITIA KATIKA ARDHI ALIYOACHIWA NA MUMEWE.



Na Mwandishi wetu,Songwe

SIKU chache baada ya mahakama ya Rufaa Kanda ya Mbeya kumpa ushindi Mjane Mariam Kalupande kuwa ndiye mmiliki halali wa eneo gombaniwa kati yake na mtoto wa shemeji yake aitwaye Rozina Kalupande lililopo kijiji cha Haraka kata ya Ezya wilayani Mbozi wadau waeleza kukoshwa na hukumu hiyo.

Kesi hiyo namba 64/2023 ya Rufaa ilifunguliwa katika mahakama kuu kanda ya Mbeya na Taasisi ya wakina mama Foundation, Kijiji cha Haraka na halmashauri ya Mbozi baada ya awali Mariamu Kalupande (MJANE) kuwafungulia kesi katika baraza la ardhi kwa kuvamiwa eneo lake.

Mzee mmoja aitwaye Isaka Mtafya mkazi wa Mbozi alisema amepong eza hukumu hiyo akisema eneo hilo ni la Leston Kalupande huku akisikitisha kitendo cha mjane Mariamu kufanyiwa ukatili kwenye eneo la famiia yake.

HISTORIA YA MZEE KALUPANDE.

Madai ya Familia ya Kalupande dhidi ya Wakina mama na watoto foundation,Familia ya Kalupande ni mwana kijiji wakijiji cha Haraka katika Wilaya ya Mbozi nchini Tanzania, Leston Kalupande ndiye baba wa familia lakini kwa bahati mbaya alifariki tarehe 17 Septemba 2012 na kuondoka,watoto, dirisha anajulika na kama Marimu Kalupande ambaye pia anaishi katika kijijikimoja.

Kabla ya 2012 Kalupande alimiliki ardhia ambapo yeye pamoja na familia yake waliiendeleza na kuendelea kuishi huko kwenye ardhi hiyo.

Awali ardhi hiyo kabla ya mzozo ilichukuliwa na Leston Kalupande kutoka kwa babu yake Shangara Halinga Mwaka 1988,Leston Kalupa nde alikuwa Morogoro akifanya kazi katika kampuni ya Kikorea iitwayo Canvas Mill Ltd ambapo alipata fedha za kuendeleza familia yake ikiwa ni pamoja na kujenga nyumba ya familia yake kijijini.

Kuna viatu vya barua jinsia livyokuwa akiwasilIna na familia yake kuhusiana na nyumba Iliyokuwa jengo katika ardhi ya migogoro,Miaka ya 1990 Leston kalupande akiwa Morogoro, alifahamiana na mwanamke wa Uswisi aliyejulikana Karin Vetter ambaye alimtembelea kaka yake ambaye alikuwa meneja wa Kampuni ya Canvas.

Marehemu Kalupande aliwaalika  rafiki Karin Vetter na wote kwa pamoja waliamua kuunda na Kusajili NGO iitwayo WAKINAMAMA NA WATOTO FOUNDATION,Leston Kalupande aliifahamisha serikali ya kijiji kuhusu mradi huo naukuaji wake na tarehe 21 Novemba, 1991.



Mkutano ulifanyika kijijini ilikuonyesha mipaka ya eneo la Leston Kalupande kwani aligombana na jirani yake hata hapo awali, The foundation ilisajiliwa mwaka 1994, kasha baada ya kuunda msingi, hapa kuwa na ofisi za NGO na Leston Kalupande waliamua kualikana kuweka ofisi katika ardhi yenye migogoro ambayo ilikuwa chini ya kazi yake.
Majengo mawili yalijengwa; moja ilitumika kama ofisi na nyingine kama ya nyumba ya wageni nyumba Baada ya mwaliko huo familia iliishi na kujishughulisha na shughuli za kiuchumi katika eneo hilo bila uingiliaji wowote.

Karin Vetter akiwa na NGO yao pamoja na Leston Kalupande walitumia ofisi yao na wageni wakijenga kwa amani bila kudai umiliki.

Kwa bahati mbaya Karin Vetter alikufa mnamo 7.12. 2004 na baada ya kifo chake familia iliendelea kutumia eneo hilo na marehemu Leston Kalupande aliendelea kutumia ofisi na jengo la wageni.

Baadaye baada ya kifo cha Leston
Kalupande tarehe 17 Septemba 2012 shughuliza NGO zilianza kuzorota lakini bado kulikuwa na mawasiliano kati ya jamaa wa Karin Vetter bodi ya wadhamini ya foundation ambao wako Uswizi na familia ya Kalupande.

Mnamo 2016 na mapema 2017 wajumbe wa bodi wasiojulika na walikuja na katiba mpya na kusajili NGO hiyo hiyo na kudai kuwa eneo hilo ni mali yao.

Mikutano liilifanywa pamoja na msingi wa bodi bila matokeo ya matunda,Familia ya Kalupande ilijaribu kusisitiza kwamba ardhi hiyo ni ya familia huku wakfuwa bodi nchini Tanzania wakisema ni mali yao.

Tarehe 26 Juni,2017 familia ilipokea barua kutoka kwa bodi ya wadhamini huko Zürich Uswisii liyosema kuacha kila msaada na mishahara ikiwa familia haita kubalikutoa ardhi kwa msingi wa bodi Tanzania.

Familia iliamua kulalamika kwa serikali ya kijijihadiofisi ya mkoa ilielekeza wilaya kusuluhisha mgogoro huo lakini haikufanya kama ilivyoelekezwa.

Mnamo Agosti 30, 2017 ofisi ya mtendaji wa kijiji kikao kiliongozwa na mkuu wa wilaya ya Mbozi na kikao haikuletamatokeo yoyote na kamishna akaiambia familia iondoke eneo hilo,Familia ya Kalupande bado ilishiakilia kuwa ardhi ni ya familia kasha kamishna alimuagiza afisa ardhi wa Wilaya ya Mbozi kupima ardhi, kugawa upya na kusajili katika Jina la Wakina mama nawatoto foundation Tanzania.

Kwa mshangao mwezi Oktoba kwa serikali ya kijiji ilitoa cheti cha hati ya kimila kwa mtua nayejulikana kama wakina mama na watoto foundation Tanzania nchini na ilisajiliwa tarehe 14 Septemba 2017 kwa usajili Na 147/MBZ/32948.

Akizungumza kwa masikitiko mjane Mariam Kalupande alisema yeye ni masikini lakini yupo tayari kuipamhaki yake popote na mungu atamsaidia kwani ardhi nimali ya familia.

Anasema mwaswahiba anayopitia ynafanywa na shemeji yake Rozina Kalupande ambaye ameukana uraia wa Tanzania na kuchukua uraia wa Uswiss bila kujali shida alizopitia na mumewe kumsomesha na kumlea.

Shari Kalupande kwa upande wake alisema ardhi hiyo ni mali yao waliyoachiwa na mareheu baba yao huku mama Mariam ndiye msimamizi mkuu anashangaa kuona wanafanyiwa fitina wakati shirika lilianzishwa wakati ardhi ipo na muasisi wa shirika ndiye mwenye ardhi.

Anasema baba wakati wa uhai wake alimchukua mdogo wake Rozina kwa jina lingine zaina witison Kalupande, mnamo mwaka 2001 alikuja baba yake mzazi kwa ambaye ni baba mdogo wa Leston Kalupande ili amsaidie Mwanae zaina Rozina kusomeshwa.

2004 alimpelekwa Shule ya sekondari mbagatuzinde huko wilayani ileje akiwa mikononi mwa leston Kalupande ambaye alikuwa akimwita kaka.

Anasema 2007 alimaliza sekondari toka mwanzoni hakuwahi kuishi nyumbani kwao tena bali Aliishi nyumbani kwa kaka yake pamoja na familia yake na mwaka 2008 alipelekwa songea kumaliza masomo yake kwa sababu hakufauli kidato cha nne.

Anasema nako huko hakuweza kumaliza masomo baada ya kudaiwa kufanya vitendo vya utovu wa nidhamu kwa wanafunzi wenzake wanafunzi mwenzie na kuchukua nguo zao pamoja na pesa kwenda moja kwa moja Dar es Salaam,

Alipofika Dar es salaam alikutana na kijana wa kiswiss aliye kuwa anafanya kazi kwenye project ya maji pamoja na Leston Kalupande kwenye shirika la Wakina mama na watoto.

Leston Kalupande ambaye ni kaka yake alikuja tambua baad ya miezi miwili alipo pigiwa simu na masista (kikatoliki ) kutoka shule ya sekondari kuwa ametoroka na hayupo Shule, kaka yake aliumia kwa sababu alitoka kulipia Ada ya shule mwezi mmoja ulio pita.

Anaongeza kuwa,hata hivyo haikuwezekana yeye kurudi Shule kwa sababu ya utovu wa nidhamu.

Baada ya hapo alipoona kaka yake amekasirika ndio akaanza taratibu za kumfuata kijana wa kizungu ulaya na ndio ilikuwa safari yake ya kwenda Uswiss.

Anasema alikaa mwaka mmoja Uswiss baadaye alirudi kuomba msamaha kwa kaka yake hapo alikuwa bado sio mwanasherika wa wakina mama na watoto.

Anasema baada ya hapo mwaka 2013 alifunga ndoa na harusi yake ilifanyika nyumbani kwa kaka yake lakini kwa bahati mbaya Leston Kalupande alikuwa ilipofika 2017 alifariki dunia.

Anasema baada ya hapo Rozina alialikwa rasimi kuwa mwana chama wa shirika la Wakina mama na watoto Uswiss na mpaka hivi leo ni mwana chama hai wa shirika kwa upande wa Uswiss na ndiye anayetajwa kuongoza zoezi la kuitaka ardhi hiyo akidai ni mali ya shirika.

Rozina kwa jina lingine zaina witison Kalupande, mnamo mwaka 2001 alikuja baba yake mzazi kwa ambaye ni baba mdogo wa Leston Kalupande ili amsaidie Mwanae zaina Rozina kusomeshwa.

Anaongeza kuwa toka 2007 amemaliza sekondari toka mwanzoni hakuwahi kuishi nyumbani kwao tena bali Aliishi nyumbani kwa kaka yake pamoja na familia yake.

Anasema kwa eneo hilo ni mali yao limetumika na familia kwa zaidi ya miaka 35 hadi sasa wanaishi hapo na makaburi yapo hapo likiwemo la Baba yao Leston Kalupande,aliyeipata ardhi hiyo kutoka kwa baba yake Shangari Halinga.





Anasema katika eneo hilo,wakifanya shughuri za kiuchumi na wakipigania kesi hiyo kwa zaidi ya miaka 7 huku mashamba yao ya parachichi na kahawa yakifyekwa na watu wasiojulikana.

Comments

Popular posts from this blog

KAEGELE NA KAZUKAMWE WAIBUKA KIDEDEA KURA ZA MAONI CCM WILAYANI NKASI

DIWANI KATA YA KALA AFARIKI DUNIA KWA UGONJWA WA KIHARUSI

Mke wa Mchungaji wa kanisa la EAGT ajinyonga akihofia deni lake la fedha za kanisa