Watekelezaji wa miradi watakiwa kuzingatia ubora na thamani ya fedha
Mkuu wa wilaya ya Nkasi Mkoani Rukwa Peter Lijualikali, amewaagiza mafundi wanaotekeleza mirada ya ujenzi wa Madarasa na vyoo katika Shule za Msingi Misunkumilo na Isunta kuzingatia muda na ubora ili kuendana na thamani ya Fedha za Serikali.
Maagizo hayo ameyatoa January 5, 2026, katika ziara yake alipotembelea shule hizo ili kujionea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa miradi hiyo.
Amesema serikali inatoa pesa nyingi ili kukamilisha miradi mbali mbali katika sekta ya elimu, ili kuwezesha mazingira yenye ubora ya watoto kupata elimu.
Sambamba na hayo amewataka wataalamu na wasimamizi wa miradi hiyo kusimamia ipasavyo na kuhakikisha inakamilika kwa wakati na inaendana na thamani ya pesa.
Katika hatua nyingine Mhe. Lijualikali amewasisitiza Walimu kutumia maeneo ya Shule zao kulima mazao ya chakula kama Mahindi ili wanafunzi wayatumie kwa chakula .
Hata hivyo amewaonya Walimu kutotumia sehemu kubwa ya maeneo ya Shule kufanya shughuli za kilimo badala yake watumie eneo kubwa kwa ajili kulima mazao ya chakula kwa ajili ya wanafunzi.




Comments
Post a Comment